ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Vodacom Tanzania Yazindua Huduma ya Bima ya Afya kupitia mfumo wa M-Pesa

I am Krantz by I am Krantz
May 14, 2022
in HABARI
0
Vodacom Tanzania Yazindua Huduma ya Bima ya Afya kupitia mfumo wa M-Pesa
0
SHARES
22
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Mkurugenzi wa Mpesa , Epimack Mbeteni akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya VodaBima “Linda afya na VodaBima” uliofanyika jijini Dar es salaam, Vodacom kwa kushirikiana  na kampuni za Jubilee Insurance ,Mo Assurance pamoja na Milvik Tanzania watatoa huduma za bima ya afya inayolenga  kutumia  mfumo wa kidijitali katika utoaji wa huduma za afya jumuishi nchini

RelatedPosts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

May 21, 2022

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

May 21, 2022

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

May 21, 2022
Load More

ADVERTISEMENT

Meneja Masoko wa M-Pesa, Noel Mazoya akizungumza kabla ya uzinduzi wa huduma ya VodaBima “Linda afya na VodaBima”  kwenye ofisi za makao makuu ya Vodacom jijini Dar es salaam

Mkurugenzi wa M-pesa , Epimack Mbeteni (wa pili kulia) akiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Jubilee Insurance, Dinpankar Acharya (kushoto), Meneja wa Utekelezaji Sheria na Kushughulikia Malalamiko (TIRA), Okoka Mgavilenzi (watatu kulia), Afisa  Bima Mkuu Mo Assurance, Pamela Ndosi (wa pili kushoto),  mkuu wa Kitengo cha Mauzo Milvik, Ismail Simanga (Watatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja ya uzinduzi rasmi wa huduma ya  VodaBima “Linda afya na VodaBima”

 

Huduma hiyo mpya chini ya VodaBima ni kwa ushirikiano na Jubilee Insurance, Mo Assurance na Milvik Tanzania.

 

13 Mei 2022, Vodacom Tanzania Plc, kampuni inayoongoza kwa huduma za teknolojia na mawasiliano, nchini leo imetangaza ushirikiano na Milvik kutoa huduma za bima ya afya kutoka Jubilee Insurance na Mo Assurance inayolenga  kutumia dijitali katika utoaji wa huduma za afya jumuishi.

Upanuzi huu unakuja baada ya kampuni hiyo kufanikiwa kwa bidhaa zake za bima ya magari kupitia VodaBima ambayo inatoa huduma za bima kubwa na ndogo kwa ushirikiano na kampuni 10 zinazotoa huduma za bima wanaoongoza nchini, jambo ambalo litawezesha Watanzania kupata huduma muhimu za afya.

Vifurushi vya bima ya Afya kutoka kwa washirika hawa vitaweza kuwafikia kwa urahisi wateja na vinapatikana kwenye huduma za Vodacom M-Pesa. Vifurushi hivyo ni vya bei nafuu na vinatarajiwa kurahisisha mchakato wa matibabu ya afya nchini. Vifurushi vilivyoanzishwa ni pamoja na malipo wagonjwa wanaolazwa hospitalini, ajali, maisha na bidhaa iliyounganishwa (Faraja Yangu) ambayo hutoa faida na kwa wengine, kwa kuwahusisha watu wazima na watoto na hutofautiana kwa bei kulingana na umri wao na virufushi maalum.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Vodacom M-Pesa, Epimack Mbeteni    alisema, “Tuna furaha kubwa leo kuweza kutangaza maendeleo haya muhimu katika utoaji wa bima kwa Watanzania. Vodacom Tanzania imeweka mkazo mkubwa kwenye afya kama kichocheo kikuu cha shughuli zetu zinazoongozwa na malengo. Huduma ya afya ni hitaji la msingi kwa Watanzania wote na tunaamini inapaswa kupatikana kwa urahisi kwa wote, hivyo ushirikiano wetu na Milvik, Jubilee na Mo assurance utasaidia kufungua hitaji hili.”

Vodacom imekuwa ikishiriki kikamilifu katika utoaji wa huduma za afya nchini kwa miaka mingi, imeweza kutoa msaada katika maeneo tofauti kama vile matibabu ya fistula ya uzazi, msaada na matibabu kwa watoto wachanga na familia zao. Mwezi uliopita, kampuni pia ilifanikiwa kuzindua mpango wake wa m-mama kusaidia wanawake wajawazito wanaopata dharura wakati wa kujifungua.

Vifurushi hivi vya bima ya afya vinakuja kufuatia mapokezi chanya ya bima ya magari iliyoanzishwa mapema mwaka huu kwa ushirikiano na kampuni 10 za bima ambapo sasa Watanzania watafurahia urahisi wa kununua bima kutoka eneo lolote nchini bila adha ya kutembelea ofisi za wakala yeyote wa bima.

Vodacom Tanzania PLC inaendelea kufanya kazi ya kutoa suluhu za kibunifu zaidi kwa wateja wake, juhudi ambazo hivi karibuni zimeiwezesha kupata tuzo ya mtoa huduma bora ya mtandao wa simu kutoka Tume ya TEHAMA nchini.

Kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Meneja Utekelezaji Sheria na kushughulikia malalamiko (TIRA), Okoka Mgavilenzi alisema serikali inahimiza matumizi ya teknolojia katika kupata na kutoa huduma muhimu za kidijitali ikiwemo bima. “Tunaipongeza Vodacom Tanzania kwa kuja na ubunifu huu na kuchukua hatua kubwa ya kuongeza watoa huduma wengi wa bima kwenye mtandao wa kidijitali wa VodaBima ambao tunaamini utaongeza kwa kasi kikubwa upatikanaji na matumizi ya huduma ya bima nchini hasa katika eneo la afya ambayo umezindua leo,” alisema Mgavilenzi.

Mkuu wa Kitengo cha Mauzo Milvik, Ismail Simanga alisema tukio hilo lilikuwa hatua kubwa sana ambayo itashuhudia afya ya famiia ikilindwa vyema na bima bora ya afya. “Afya na usalama wa famila yako inamaanisha ulimwengu kwako. Tunaelewa na tunataka kukusaidia kuwalinda wapendwa wako dhidi ya hali zilizo nje ya uwezo wako”.

Kupitia jukwaa la MPesa watanzania wataweza kupata bima zetu popote pale walipo bila tabu yoyote.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA
HABARI

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA
HABARI

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI
HABARI

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA
HABARI

ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA
HABARI

BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In