ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NMB YAZINDUA KIFURUSHI MAALUM KWAAJILI YA WALIMU

I am Krantz by I am Krantz
Jun 23, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
NMB YAZINDUA KIFURUSHI MAALUM KWAAJILI YA WALIMU
0
SHARES
21
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Afisa Mkuu Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB, Filbert Mponzi (watatu kushoto) akimpa maelezo Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuzindua Mpango maalum  ‘Mwalimu Spesho’ uliyozinduliwa jana Jijini Dodoma. Wapili kushoto ni Mkuu wa Idara ya wateja Binafsi, Aikansia Muro na Meneja kanda ya Kati Nsolo Mlozi.
Afisa Mkuu Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kushoto)  akishirikiana na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kutoa kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua Mpango maalum wa ‘Mwalimu Spesho’ iliyozinduliwa jana Jijini Dodoma.

 

 

RelatedPosts

Benki ya NMB yasaidia ukusanyaji wa Trilioni 8.6 za Serikali

Benki ya NMB yasaidia ukusanyaji wa Trilioni 8.6 za Serikali

Jun 23, 2022

NMB yakabidhi Vifaa vya Usafi – Dodoma

Jun 16, 2022

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna ashinda tuzo ya Mkurugenzi Mtendaji Bora wa Kibenki Barani Afrika 2022 (Tanzania)

May 29, 2022
Load More

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ametoa Rai kwa benki ya NMB kuhakikisha inawafikia watumishi wengi zaidi wakiwemo walimu ili kuwasaidia kujiendeleza kimaisha.

Kauli hiyo aliitoa jana wakati akizungumza na walimu wa Shule za Msingi na Sekondari wa kanda ya Kati Jijini  Dodoma katika siku ya Mwalimu iliyoandaliwa na benki ya NMB ikienda sambasamba na uzinduzi wa Mpango wao  Maalum wa “Mwalimu Spesho.”

Mpango huo ni kwa ajili ya walimu kupata mikopo na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo nchini huku walimu wakipongeza huduma hizo.

ADVERTISEMENT

Waziri alisema mpango huo mzuri usiishie kwa walimu 5,000 badala yake angetamani uwafikie walimu wengi na watumishi ili kuwajengea uwezo hasa walimu ambao ndiyo chanzo cha kuwaandaa viongozi, wataalamu wa baadae.

Alitaka NMB kusimama na walimu wakati wote ili kuwajengea uwezo akieleza kuwa jumla ya walimu 6800 wamepandishwa madaraja hivyo ni fursa kwao kuingia kwenye mikopo kwa benki ambayo inajulikana na uendeshaji wake mzuri kuliko kukopa kwenye taasisi ambazo zinawaumiza.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi alisema walikusanya walimu viongozi 350 kwa ajili ya kubadilishana mawazo kuboresha zaidi huduma za kibenki na kujadiliana kuhusu fursa zilizopo kwa ajili ya kundi la Walimu nchini.

“Tunaamini, walimu hawa zaidi ya 350, watasaidia kupeleka elimu watakayoipata hapa kwa wenzao na hata familia zao na jamii kwa ujumla juu ya huduma nzuri zinazotolewa na benki ya NMB, lengo ni kumfanya mwalimu kuwa na maisha mazuri wakati wote,” alisema Mponzi.

Hoja ya NMB ilianzia kwa mbunge wa Viti Maalumu, Dkt. Teya Ntala ambaye aliomba mabenki mengine kuiga mfano wa benki hiyo kwani imekuwa ni sehemu ya kuigwa mfano kwa wanyonge.

Aidha, Benki ya NMB inatoa mikopo mingi ikiwemo bima ya kujikinga na majanga mbalimbali, mikopo ya elimu kwa walimu na wategemezi wake, mikopo ya kilimo,uvuvi na ufugaji, mikopo ya vyombo vya moto vya binafsi na biashara na mikopo ya wakulima wadogo wadogo.

**********

*Mwisho*

ADVERTISEMENT

 

 

 

Related

Tags: NMB
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Auto Draft
HABARI

NBC Wanogesha hafla ya kukabidhiwa Kombe Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC, klabu ya Yanga SC j

by I am Krantz
Jun 26, 2022
ROSE REE AFUTE PICHA ZOTE ZA  MCHUMBA WAKE
HABARI

ROSE REE AFUTE PICHA ZOTE ZA MCHUMBA WAKE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
KAJALA ATOA AHAADI NZITO KWA HARMONIZE
HABARI

KAJALA ATOA AHAADI NZITO KWA HARMONIZE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
HUYU NDIYO MWENYE WAFUASI WENGI ZAID TIKTOK
HABARI

HUYU NDIYO MWENYE WAFUASI WENGI ZAID TIKTOK

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
ALICHO KISEMA LUKAMBA KUHUSU HARMONIZE
HABARI

ALICHO KISEMA LUKAMBA KUHUSU HARMONIZE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
CRDB BANK PAMOJA BONANZA ILIVYOFANA JIJINI DODOMA
BIASHARA

CRDB BANK PAMOJA BONANZA ILIVYOFANA JIJINI DODOMA

by I am Krantz
Jun 26, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In