ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Alichozungumza Mbowe na diaspora

I am Krantz by I am Krantz
Jun 5, 2022
in HABARI
0
Mbowe awakumbuka kina Mdee
0
SHARES
99
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema Watanzania wanahitaji katiba mpya ambayo itatengeneza mfumo bora wa utawala wa nchi badala ya kuacha kila uamuzi kufanywa na Rais.

Mbowe aliyasema hayo jana Jumamosi Juni 4, 2022 wakati akizungumza na Watanzania waishio nje ya nchi (diaspora) kwa njia ya teknolojia akiwaeleza masuala mbalimbali ya kitaifa pamoja na mipango ya chama chake.

RelatedPosts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

Mar 24, 2023

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

Mar 24, 2023

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

Mar 24, 2023
Load More

Alisema Chadema kina mpango mzuri wa kurudisha madaraka kwa wananchi na kuondoa mifumo yote inayoelekeza mamlaka kwa watu wachache au mtu mmoja kuamua juu ya maisha ya Watanzania zaidi ya milioni 60.

“Sisi Chadema tunahitaji ku-decentralize (ugatuzi), nchi nyingi wamefanya hivyo. Tanzania tunaweza tukaanzisha kanda 10 kama za Chadema na zikawa zone na Serikali yake na Bunge lao dogo linalojitegemea na kujipangia sheria zao.

“Kwa hiyo lazima twende kwenye kanda au majimbo…wanakuwa na magavana wao na wanachaguliwa na wananchi, sio watu wa kuteuliwa. Unateua mtu ambaye hana attachment yoyote na wale watu anakwenda kuwaongoza, hilo linatakiwa kukomeshwa,” alisema.

Alisisitiza kwamba hakuna mkoa ulio masikini hapa nchini, kwa sababu kila mkoa una utajiri wa rasilimali zake, hata ile mikoa iliyotambulika kuwa masikini kama Mtwara na Lindi, ina utajiri mkubwa.

“Lazima tu-address wapi tunapokwama mambo ya msingi, tunajikwamuaje kwa kuiangalia katiba, mifumo yetu ya utawala, utawala uwe kwa watu, watu waamue viongozi wao, wawachague viongozi wao.

“Katiba ihakikishe kwamba tunajenga taasisi imara, mabunge katika kanda ambayo yanawajibika, mabunge yatakayoangalia maslahi ya wananchi. Tunahitaji mahakama ambayo ni huru. Lazima tuwe na katiba ambayo itaweka makatazo,”alisema Mbowe.

ADVERTISEMENT

Suala la elimu

Mbowe alisema Tanzania inahitaji kufumua mfumo mzima wa elimu kwa sababu watu wengi bado wamelemaa na mfumo wa vyeti, ndiyo maana kumekuwa na wizi wa mitihani shuleni na vyuoni.

“Wakishaingia Wakenya, Wazimbabwe na Waganda, tunapoteza. Zinakuja multinational companies zinalazimika kuajiri watu kutoka Afrika Kusini lakini wanashindwa kuwachukua vijana kutoka Dar es Salaam licha ya kwamba ni nafuu kwa maana ya gharama za uendeshaji,” alisema.

Alisisitiza kwamba Kiswahili ni kizuri kutumika lakini kisiitoe Tanzania katika ulimwengu wa ushindani ambao nayo iko ndani yake. Alisisitiza kwamba kama Tanzania haiwezi kushindana katika mchangamano na mataifa mengine basi hakuna manufaa yoyote.

“Unakuta hawa watunga sera wetu wanakwambia tufundishe Kiswahili kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu, sawa, lakini ni watu hao hao ambao wanawapeleka watoto wao katika shule za English Medium.

“Wanawapeleka watoto wao kusoma Afrika Kusini, China, Uingereza, ili mradi wapate ile exposure. Hata wakisoma ndani ya nchi, wanasoma katika shule ambazo ni za English Medium,” alisema Mbowe.

Alisema watoto ambao wanasoma kwa lugha za kigeni kama Kiingereza wanafanya vizuri hata katika soko la ajira, ndiyo maana ukienda mataifa ya Dubai utawakuta Wakenya wengi au raia wa Afrika Kusini.

ADVERTISEMENT

Hoja ya maridhiano

Mwenyekiti huyo wa Chadema alisema maridhiano imekuwa ni sehemu ya uendeshaji wa chama hicho kwa miaka mingi lakini Serikali ya awamu ya tano haikutaka maridhiano kwa sababu iliamini upinzani ni tishio.

Alisema baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuingia madarakani, Chadema walikuwa na shauku ya kuzungumza naye, walimwandikia barua ya kuzungumza naye wakiamini kwamba wanahitaji kuwa na maridhiano.

Mbowe alisema hata alipotoka gerezani baada ya kuachiwa, hakusita kupokea wito wa Rais Samia alipomtaka kwenda kuzungumza naye Ikulu. Alisema anaona dhamira njema katika majadiliano ambayo wamekuwa wakifanya baina ya chama chake na CCM.

“Niseme wazi kwamba hadi wakati huu nimeona dhamira njema ya Rais Samia katika mazungumzo ambayo tumeyafanya na tutaendelea na mazungumzo hayo kwa awamu tofauti. Kama dhamira hiyo itaondoka basi hatutasita kujiondoa kwenye mazungumzo hayo,” alisema.

Mwanasiasa huyo mkongwe aliwataka wanachama wa Chadema kuwa wavumilivu wakati majadiliano hayo yanaendelea huku akiwahakikishia kwamba kila kitu kitakwenda vizuri kwa maslahi ya chama chao.

Mgogoro NCCR Mageuzi

Akizungumzia mgogoro ndani ya NCCR Mageuzi, Mbowe amesema Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imekuwa ikiingilia masuala ya ndani ya vyama vya siasa na kusababisha mgogoro ambayo inadhoofisha vyama.

Aliitaka ofisi hiyo isiingilie masuala ya uendeshaji wa vyama nchini bali ivilee na kuvisimamia bila kuviingilia na kusababisha mifoforo ndani yake kama ilivyotokea hivi karibuni ndani ya NCCR Mageuzi.

Wadau wengine

Akichangia kwenye mjadala huo, mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Azavery Lwaitama alisema amefurahishwa na suala la ugatuzi wa mamlaka ya dola ambao siyo kwa Tanzania Bara na Zanzibar bali kuigawa Tanzania katika kanda zake.

Alisema anakubaliana na hoja ya Mbowe kwamba Chadema ni chama cha wote, wajamaa na wasio wajamaa, hivyo, ni muhimu kuvumiliana katika kufanya siasa ndani ya nchi.

“Chama kilianzishwa na mtu aliyekuwa anabishana na Nyerere lakini mzalendo na Mwalimu Nyerere alikubali kuwa ni mzalendo.

Umeliweka vizuri kwamba Chadema ni chama cha wote na kila mtu ana haki ya kuwa mwanachama wa Chadema bila kujali ni mjamaa au siyo mjamaa, alisema Dk Lwaitama wakati akichangia kwenye mjadala huo.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE
HABARI

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA
HABARI

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII
HABARI

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI
HABARI

WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI
HABARI

MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC
HABARI

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC

by I am Krantz
Mar 24, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In