Klabu ya Liverpool ipo tayari kumuachia mshambuliaji wake Sadio Mane, ajiunge na klabu ya Bayern Munich ya nchini Ujerumani kwa dau la pauni milioni 40.
–
ADVERTISEMENT
Mane mwenye umri wa miaka 30, amekuwa akishinikiza kutaka kuondoka wakati huu wa majira ya kiangazi.
–
ADVERTISEMENT
Liverpool watakubali kuchukua kiasi hicho cha pesa ili kutunisha kibubu chao waweze kuinasa saini ya Darwin Nunez ambaye anatajwa kuwa na thamani ya pauni milioni 60.