ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Makada 19 wa Chadema waachiwa huru Mwanza

I am Krantz by I am Krantz
Jun 1, 2022
in HABARI
0
Makada 19 wa Chadema waachiwa huru Mwanza
0
SHARES
89
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

HATIMAYE LISSU AREJEA TENA NCHINI

HATIMAYE LISSU AREJEA TENA NCHINI

Jan 25, 2023

Hatima ya Mazungumzo Kati ya CHADEMA na CCM Itajulikana

Nov 29, 2022
Load More

Mwanza. Viongozi na wanachama 19 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la kufanya fujo kwenye mkusanyiko wa kidini katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kawekamo jijini Mwanza wameachiwa huru.

Washtakiwa hao wameachiwa huru leo Juni Mosi, 2022 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza,  Bonaventure Lema baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo namba 77/2021.

Kwa mara ya kwanza makada hao walifikishwa mahakamani Agosti 19, 2021 wakidaiwa kutenda kosa hilo Agosti 15, 2021 baada ya kuhudhuria ibada ya Jumapili katika Kanisa Katoliki parokia ya Kawekamo wakiwa wamevaa sare za chama chao na fulana nyekundu zilizoandikwa Katiba Mpya.

Walioachiwa huru ni pamoja na Katibu wa Chadema Kanda ya Victoria, Zakaria Obadi, Deus Shinengo, mang’ombe Oswald, Kelvin John, Farida Gilala, John Nyamhanga, Emmanuel Mtani na Frank Nyamuga.

Wengine ni Msafiri Nteminyanda, Musa Kimweri, Gadson Jacob, Elieza Mkungu, Dionise Edward, Michael Christian, Leah Joseph, James Mayala, Yasinta Wachelele na Eudia Frank. Washtakiwa wote walikuwa wanawakilishwa na Wakili Erick Muta.

Akisoma hati ya mashtaka wakati shauri hilo lilipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Agosti 19, 2021, Wakili wa Serikali, Bisela Bantulaki alidai mbele ya Hakimu Mkazi Emmanuel Lukumay kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Agosti 15, 2021 katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kawekamo Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza.

Wakili Bantulaki alidai kwa pamoja, washtakiwa ambao wote walikana mashtaka dhidi yao walifanya fujo wakati ibada ya matoleo ikiendelea.

Washtakiwa wote walikuwa nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya mdhamini aliyesaini hati ya dhamana ya Sh1 milioni, barua ya utambulisho kutoka ofisi ya Serikali ya Mtaa na nakala ya kitambulisho cha mpigakura au cha Taifa.

CHANZO; MWANANCHI

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: CHADEMA
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE
HABARI

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA
HABARI

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII
HABARI

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI
HABARI

WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI
HABARI

MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC
HABARI

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC

by I am Krantz
Mar 24, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In