ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, February 7, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Makocha Kutoka Sehemu Mbali Mbali Duniani Wamiminika Kutaka Kibarua Cha Pablo Simba

I am Krantz by I am Krantz
Jun 3, 2022
in HABARI, MAGAZETI TANZANIA
0
PABLO AWATUPIA LAWAMA WACHEZAJI WAKE
0
SHARES
106
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

KLABU ya Simba imesema kuwa imepokea maombi kwa simu na barua pepe kutoka kwa mawakala na makocha mbalimbali duniani wakitaka kibarua cha kuifundisha timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao, baada ya kumtimua kocha wao Pablo Franco.

Pamoja na hayo, klabu hiyo imesema imekuwa ikiingia makubaliano na baadhi ya wachezaji, lakini haijaanza rasmi usajili hadi hapo itakapitia ripoti ilioachwa na kocha aliyepita, lakini na mapendekezo ya kocha mpya atakayekuja.

RelatedPosts

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Feb 7, 2023

HAJI MANARA AIJIA JUU BODI YA LIGI KISA CLEAN SHEETS, SIMBA SC

Feb 7, 2023

DAYOO AFUNGUKA KWANINI ANASEMA “NAITWA MANGI…”

Feb 7, 2023
Load More

Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally amesema jana tangu ilipoachana na kocha Pablo na kutangaza rasmi Mei 31, imekuwa ikipata maombi kutoka kwa makocha mbalimbali kurithi mikoba yake.

“Kuna wakati kila baada ya saa moja tunapata simu pamoja na barua pepe, lakini tangu kocha aondoke tumepata maombi mengi kutoka kwa mawakala ambao wamekuwa wakituambia wana makocha wazuri, pia makocha wenyewe kutoka pande mbalimbali za dunia wamekuwa wakitupa wasifu wao ili tu kuisaka kazi ya kocha aliyepita.

Kumiminika kwa maombi haya siyo kwamba kuna uhaba wa ajira la hasha, ila ni kwa ajili ya ukubwa na Simba, kila kocha mkubwa na mwenye viwango angependa kuja kuifundisha Simba, lakini hiyo haitufanyi sisi tuingie kwenye presha hizo, tutakaa na kuangalia nani atatufaa.

Hata sisi tunafuatilia mpira tunafahamu makocha wazuri, kwa hiyo atakayekidhi vigezo ndiyo atakayekuwa kocha wa Simba na tunawaahidi wanachama na mashabiki wa Simba tutawaletea kocha mwenye viwango vya dunia.” Alisema.

ADVERTISEMENT

Kuhusu usajili alisema harakati za kuingia makubaliano zimeanza, lakini hawajaanza usajili rasmi.

ADVERTISEMENT

“Usajili hatujaanza rasmi, tumeelekeza jicho kusaka kocha, tukimpata kocha ndani ya wiki hizi mbili, ndiyo tutaanza mipango ya kukaa na kocha kutuambia anataka wachezaji wa aina gani na yeye aone wachezaji waliopo. Mapendekezo ya kocha aliyepita na kocha mpya ndiyo yatatuelekeza na kutupa mwanga na taswira ni aina gani ya wachezaji ambao tunakwenda kuwasajili.” Alisema Ahmed.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA
HABARI

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
TANZANIA, UAE ZASAINI KUHIFADHI MAZINGIRA
HABARI

TANZANIA, UAE ZASAINI KUHIFADHI MAZINGIRA

by ALFRED MTEWELE
Feb 7, 2023
YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25
HABARI

HAMTAMUONA KOCHA NABI AIRPORT – ALLY KAMWE

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25
HABARI

YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
QUEIROZ KOCHA MPYA QATAR
HABARI

QUEIROZ KOCHA MPYA QATAR

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
ATSU APATIKANA AKIWA HAI KUTOKA KWENYE VIFUSI
HABARI

ATSU APATIKANA AKIWA HAI KUTOKA KWENYE VIFUSI

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In