Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amemuhamisha Katibu mkuu wa Wizara ya Utalii na Maliasili, Dkt. Francis Michael kwenda wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kuchukua nafasi ya Eliamani Sedoyeka aliyehamishiwa wizara ya Utalii na Maliasili.
–
Ingawa, taarifa ya Ikulu, kuhusu mabadiliko hayo haijasema sababu za mabadiliko ni nini, baadhi ya maoni ya watu yanahusisha na kile kinachoendelea huko Loliondo na Ngorongoro.
–
Michael alikuwa mtendaji mkuu wa wizara ya maliasili na Utalii, inayosimamia masuala ya hifadhi za nchi hiyo ikiwemo ya Ngorongoro na Pori Tengefu Loliondo, kaskazini mwa Tanzania, zilizoibua wasiwasi wa kiusalama hivi karibuni.