ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Serikali Kununua Silaha za Raia Kuepusha Vifo Holela

I am Krantz by I am Krantz
Jun 1, 2022
in HABARI
0
Serikali Kununua Silaha za Raia Kuepusha Vifo Holela
0
SHARES
38
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

Auto Draft

NBC Wanogesha hafla ya kukabidhiwa Kombe Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC, klabu ya Yanga SC j

Jun 26, 2022

ROSE REE AFUTE PICHA ZOTE ZA MCHUMBA WAKE

Jun 26, 2022

KAJALA ATOA AHAADI NZITO KWA HARMONIZE

Jun 26, 2022
Load More

Serikali ya Canada inatarajia kupitisha sheria mpya inayopiga marufuku uuzaji, ununuzi, uingizaji na uhamisho wa bunduki, sambamba na mpango wa kununua silaha zinazomilikiwa na raia wake ili kudhibiti matukio holela ya kiuhalifu nchini humo.

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema hatua hiyo inafuatia uwepo wa matukio kadhaa ya kiuhalihu ikiwemo lile la vifo vya watu 22 waliouwawa katika kijiji cha Nova Scotia na mtu mwenye bunduki mwaka 2020.

“Kama serikali na kama jamii tuna jukumu la kuchukua hatua ili kuzuia majanga zaidi tunahitaji kujua ikiwa hatutachukua hatua kwa uthabiti na kwa haraka itakuwa mbaya zaidi na ngumu zaidi kukabiliana nayo,” amesema Trudea.

Mpango huu unaakisi ule uliochukuliwa na nchi ya New Zealand mwaka 2019 baada ya mtu aliyejihami kwa bunduki kuvamia misikiti miwili na kuuwa watu 51 na kujeruhi wengine kadhaa katika kanisa la Christchurch.

Shambulio jingine ni lile la vifo vya watu wengi nchini Australia mwaka 1996 lililoifanya Serikali ya nchi hiyo kukusanya zaidi ya bunduki 650,000 za semiautomatic na zile za aina nyingine kisha kupiga marufuku matumizi ya silaha chini ya sheria mpya.

Matumizi ya silaha kinyume na matarajio yamekuwa yakitokea katia maeneo mengi Duniani ambapo kwa nchini Tanzania novemba 2013 mfanyabiashara Gabriel Munisi (35), alijiua kwa risasi baada ya kumuua mtu mmoja na kujeruhi wengine watatu jijini Dar es Salaam katika tukio lililohusishwa na wivu wa mapenzi.

Tukio hilo lilitokea ikiwa ni mwezi mmoja (Oktoba, 2013), baada ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa ITV Ufoo Saro kujeruhiwa na mama yake mzazi kuuliwa kwa risasi na mzazi mwenzake Anthery Mushi ambaye naye alijiua katika tukio lililosababishwa na masuala ya kimapenzi.

Mei 27, 2017 Maxmilian Tula (40), mkazi wa Kanyenyere kata ya Butimba jijini Mwanza alimuua mkewe Teddy Malulu kwa kumpiga risasi kisha na yeye kujiua kwa kujipiga risasi.

Aidha Mei 30, 2022 Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Mairi Makori amethibitisha kifo cha mtuhumiwa Said Oswayo aliyejipiga risasi akidaiwa kumuua mkewe Swalha Salum (28), kwa kumpiga risasi kadhaa mwilini.

“Mwili huo umeopolewa ziwani eneo la ufukwe wa Rock Beach ukiwa na majeraha ya risasi kichwani na tumejiridhisha kuwa ndiye mtuhumiwa baada ya kutambuliwa na ndugu zake,” amesema Makori.

Julai 2021 Dar 24 iliripoti tukio la mwanaume mmoja Jonathan Gachunga(42), kumuua mkewe na kisha baadaye kujipiga risasi kichwani nyumbani kwao Kaunti ya Kiambu nchini Kenya.

Mamlaka stahiki zinapaswa kukemea kisha kuchukua hatua zitakazoondosha matukio ya vifo vinayosababishwa na matumizi ya silaha kwani yanaacha maumivu na majonzi kwa baadhi ya familia na kuharibu mustakabali wa maisha yao

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Auto Draft
HABARI

NBC Wanogesha hafla ya kukabidhiwa Kombe Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC, klabu ya Yanga SC j

by I am Krantz
Jun 26, 2022
ROSE REE AFUTE PICHA ZOTE ZA  MCHUMBA WAKE
HABARI

ROSE REE AFUTE PICHA ZOTE ZA MCHUMBA WAKE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
KAJALA ATOA AHAADI NZITO KWA HARMONIZE
HABARI

KAJALA ATOA AHAADI NZITO KWA HARMONIZE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
HUYU NDIYO MWENYE WAFUASI WENGI ZAID TIKTOK
HABARI

HUYU NDIYO MWENYE WAFUASI WENGI ZAID TIKTOK

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
ALICHO KISEMA LUKAMBA KUHUSU HARMONIZE
HABARI

ALICHO KISEMA LUKAMBA KUHUSU HARMONIZE

by Shabani Rapwi
Jun 26, 2022
CRDB BANK PAMOJA BONANZA ILIVYOFANA JIJINI DODOMA
BIASHARA

CRDB BANK PAMOJA BONANZA ILIVYOFANA JIJINI DODOMA

by I am Krantz
Jun 26, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In