ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

TMA yatahadharisha Baridi kali Nyanda za Juu kusini

I am Krantz by I am Krantz
Jun 3, 2022
in HABARI
0
TMA yatahadharisha Baridi kali Nyanda za Juu kusini
0
SHARES
216
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

No Content Available
Load More

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mwelekeo wa kipupwe unaotarajiwa kuanza Juni hadi Agosti mwaka huu katika mikoa mitano ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi yenye miinuko, inatarajiwa kuwa baridi kali chini ya nyuzi joto nne (4 °C) .

Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti na Matumizi wa TMA, Dk Ladislaus Chang’a alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar es Salaam, akiitaja mikoa ya Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe na kusini mwa Morogoro, kuwa itaathiriwa na hali hiyo.

Lakini DK Chang’a alisema hali ya joto kiasi na baridi ya wastani inatarajiwa katika maeneo mengi nchini.

Alisema kiwango cha baridi katika maeneo hayo kinatarajiwa kuwa kati ya nyuzi joto 4 hadi 14, huku maeneo yenye miinuko yakitarajiwa chini ya nyuzi joto nne.

Akizungumzia Mkoa wa Ruvuma, Dk Chang’a alisema unatarajiwa kuwa na baridi kiasi cha nyuzi joto kati ya 6 C na 14 C, Mtwara na Lindi kati ya nyuzi joto 14 C na 22 C, Singida na Dodoma nyuzi joto 12 C na 18 C, Tabora, Rukwa, Katavi na Kigoma nyuzi joto 14 C na 18 C.

Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara inatarajiwa kuwa na nyuzi joto kati ya 10 C na 18 C, Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Kaskazini Morogoro, Unguja na Pemba nyuzi joto 18 C na 26 C wakati Mwanza, Mara, Geita, Kagera, Shinyanga na Simiyu ikitarajiwa kuwa nyuzi joto kati ya 14 C na 20 C.

“Hali ya baridi ya wastani hadi joto kiasi inatarajiwa katika maeneo mengi nchini na hali ya joto kiasi hadi baridi ya wastani inatarajiwa katika maeneo ya ukanda wa Pwani Kaskazini pamoja na nyanda za juu kaskazini mashariki na vipindi vya baridi zaidi vinatarajiwa kujitokeza kati ya Juni na Julai,” alisema Dk Chang’a.

Pia, alisema katika kipindi cha Juni na Agosti vipindi vya upepo mkali vinatarajiwa kuvuma kutoka kusini mashariki na mashariki (Matlai) katika ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na meneo ya nchi kavu, hususan Agosti mwaka huu.

Dk Chang’a alisema athari zinazoweza kujitokeza ni homa ya mapafu kwenye mifugo na binadamu.

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: TMA
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE
HABARI

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA
HABARI

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII
HABARI

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI
HABARI

WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI
HABARI

MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC
HABARI

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC

by I am Krantz
Mar 24, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In