ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, March 28, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Watumiaji wa Vodacom M-Pesa Kugawiwa Faida ya Shilingi 3.3 Bilioni

I am Krantz by I am Krantz
Jun 15, 2022
in HABARI
0
Watumiaji wa Vodacom M-Pesa Kugawiwa Faida ya Shilingi 3.3 Bilioni
0
SHARES
123
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

16 Juni 2022: Vodacom Tanzania Plc imeanza kutoa mgao wa Shilingi 3.3 bilioni kwa watumiaji wake zaidi ya 7.7 milioni, ikiwa ni sehemu ya faida iliyopatikana kwenye akaunti za M-Pesa. Malipo haya yanategemewa kukamilika tarehe 17 Juni, ambapo wateja wote watakuwa wameshapokea mgao wao na kufanya idadi itakayotolewa kwa ujumla kufikia Shilingi 174 bilioni tangu kampuni hiyo ianze kugawa faida kwa wateja wake
Akifafanua kuhusu gawio hilo la M-Pesa, Mkurugenzi wa M-Pesa Epimack Mbeteni, alisema, “tuna furaha kubwa sana kuona kuwa huduma ya M-Pesa inaendelea kuwa msingi wa shughuli za kibiashara pamoja na maisha ya kila siku ya wananchi hapa nchini. Tuko katika mchakato wa kugawa Shilingi 3.3 bilioni kwa wateja wetu ambao wamekuwa wakitumia mfumo wetu kwa kipindi hiki, na malipo yanaingia moja kwa moja katika akaunti zao za M-Pesa.”
Faida italipwa kwa wateja, mawakala, wakala mkuu na wadau wengine wa kibiashara wa M-Pesa kulingana na matumizi yao ya huduma za M-Pesa. Gawio linategemea kiasi cha matumizi ya huduma katika kipindi hicho cha robo ya kwanza ya mwaka 2022 (Januari hadi Machi). Shughuli hizo ni pamoja na kuhamisha pesa, kulipa bili, manunuzi ya muda wa maongezi na mengine.
Wateja wanaweza kutuma neno “KIASI” kwenda namba 15300 ili kuona kiasi cha gawio watakalopokea. Mara baada ya kupokea mgao, wateja wa M-Pesa wanaweza kutumia gawio hilo kwa njia ya kutoa pesa taslimu, kununua vifurushi vya maongezi na data au kutumia kulipia bili au manunuzi ya bidhaa.
Bw. Mbeteni alimalizia kwa kusema, “Mfumo huu wa kipekee umekuwa na nafasi kubwa katika kujenga hali ya ushirikishwaji na upatikanaji wa huduma za kifedha nchini. Wanawake na vijana wameona unafuu na urahisi wa kutumia M-Pesa na wanatumia huduma nyingi ili kuboresha maisha yao. Pia mfumo umekuwa rasilmali muhimu katika kuwezesha biashara ndogondogo na kupambana na changamoto zilizosababishwa na mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO -19. Kwetu Vodacom Tanzania, dhamira yetu ni kuhakikisha kuwa mfumo huu tunauboresha ili kuendana na mahitaji ya wateja wetu.”

Kuhusu Mfumo wa Vodacom M-Pesa
Vodacom M-Pesa ni mfumo mkubwa kabisa nchini wa huduma za kifedha kwenye mtandao wa simu uliozinduliwa na Vodacom Tanzania Plc mwaka 2008. Kwa sasa ukiwa umesajiliwa na shirika la GSMA na ukiwa na watumiaji zaidi ya 11 milioni, M-Pesa imeongeza kwa kiasi kikubwa ushirikishwaji kifedha pamoja na shughuli za kiuchumi nchini. Wateja wanaweka na kutoa pesa kutoka kwenye akaunti zao za M-Pesa kupitia mtandao wa mawakala Zaidi ya 108,000 nchi nzima. Mtandao wa M-Pesa unaunganisha biashara, mabenki na taasisi za serikali katika kuwezesha miamala kidijitali.

RelatedPosts

DC JOKATE MWEGELO AZURU NCHINI AFRIKA KUSINI KUTANGAZA FURSA ZAO LA MKONGE

DC JOKATE MWEGELO AZURU NCHINI AFRIKA KUSINI KUTANGAZA FURSA ZAO LA MKONGE

Mar 28, 2023

MBUNGE ATOA MAJIKO YA GESI 700 KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI

Mar 28, 2023

TAIFA STARS YAAHIDI KUENDELEZA ILIPOISHIA

Mar 28, 2023
Load More
ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

DC JOKATE MWEGELO AZURU NCHINI AFRIKA KUSINI KUTANGAZA FURSA ZAO LA MKONGE
HABARI

DC JOKATE MWEGELO AZURU NCHINI AFRIKA KUSINI KUTANGAZA FURSA ZAO LA MKONGE

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023
MBUNGE ATOA MAJIKO YA GESI 700 KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI
HABARI

MBUNGE ATOA MAJIKO YA GESI 700 KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023
RAIS SAMIA ATUNUKIWA TUZO NA WANAHABARI, JNICC
HABARI

RAIS SAMIA ATUNUKIWA TUZO NA WANAHABARI, JNICC

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023
MFAHAMU MVUVI ALIYEPOTELEA BAHARINI SIKU 438, NA KUKUTWA BADO YUPO HAI
HABARI

MFAHAMU MVUVI ALIYEPOTELEA BAHARINI SIKU 438, NA KUKUTWA BADO YUPO HAI

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023
MAKAMU WA RAIS MAREKANI ZIARANI KESHO NCHINI
HABARI

MAKAMU WA RAIS MAREKANI ZIARANI KESHO NCHINI

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023
WASANII BONGO WALIOTAJWA PLAYLISTS YA KAMALA
HABARI

WASANII BONGO WALIOTAJWA PLAYLISTS YA KAMALA

by ALFRED MTEWELE
Mar 28, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
June 2022
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In