ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, May 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NMB YATOA VIFAA VYA AFYA NA ELIMU WILAYA YA LUSHOTO

I am Krantz by I am Krantz
Jul 14, 2022
in HABARI
0
NMB YATOA VIFAA VYA AFYA NA ELIMU WILAYA YA LUSHOTO
0
SHARES
224
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Benki ya NMB imetoa msaada wa mabati 200 kwa Zahanati ya Kwemakame iliyopo wilayani Lushoto mkoani Tanga yenye thamani ya Sh. milioni 7.1 na madawati 50 katika Shule ya Msingi Mbula B iliyopo wilayani humo yenye thamani ya Sh.milioni 3.9 ambapo jumla ya msaada huo ni Sh. milioni 11.

RelatedPosts

POCHETTINO AANZA NA JOAO FELIX AREJEE ATLETICO

POCHETTINO AANZA NA JOAO FELIX AREJEE ATLETICO

May 30, 2023

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE

May 30, 2023

MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA

May 30, 2023
Load More

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper alisema kuwa benki hiyo inatambua juhudi za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Samia Suluhu Hassan za kusimamia huduma za afya na elimu kwa nguvu zote kwa kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma hizo mjini na vijijini.

Meneja huyo wa kanda alisema walipopata maombi ya kuchangia katika maendeleo ya elimu kwa Wilaya ya Lushoto walifarijika na kushirikiana nao ili ikawe chachu ya maendeleo ya sekta ya afya na elimu kwa jamii yao hasa katika zahanati ya Kwemakame na kwa Shule ya Msingi Mbula B.

Aliongeza kuwa imani yao ni kuwa vifaa hivyo vitatumika vyema kwa manufaa makubwa ya wananchi wa wilaya hiyo. ” Vifaa vinavyokwenda shuleni basi watoto wetu na wadogo zetu watakwenda kunufaika vyema kabisa na hata kusaidia ufaulu wao.,” alisema na kuongeza:

 

 

 

 

“Benki ya NMB tumekuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii, ni kwa zaidi ya miaka saba mfululizo tumekuwa tukitenga asilimia 1% ya faida yetu kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayotuzunguka, “alibainisha Prosper.

Awali akipokea msaada huo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Kalist Lazaro aliishukuru benki hiyo kwa msaada huo na kueleza kuwa msaada huo wa madawati unakwenda kuwatoa watoto wao kwenye vumbi na hatimaye sasa kukaa kwenye madawati huku mabati hayo yakienda kusaidia kwenye huduma za afya.

ADVERTISEMENT

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Ikupa Mwasioge alisema benki hiyo imekuwa ikijihusisha na utoaji wa misaada katika jamii zao kwani mbali na msaada huo hivi karibuni waliwapatia msaada wa vifaa katika kituo cha afya cha Mlalo.

ADVERTISEMENT

Mjumbe wa kamati ya shule hiyo alisema kwa niaba ya kamati ya shule na wazazi wa kijiji hicho wameishukuru benki ya NMB kwa kuwapatia msaada huo ambao unakwenda kuongeza ufaulu shuleni hapo.

“Haya mabati 200 yanakwenda kutusaidia katika Zahanati yetu ya Kwemakame kuezeka kwani ilijengwa na bado haijaezekwa mabati, “alisema William Aloyce – Mtendaji wa Kijiji cha Kwemakame Kata ya Kwai.

MWISHO

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

POCHETTINO AANZA NA JOAO FELIX AREJEE ATLETICO
HABARI

POCHETTINO AANZA NA JOAO FELIX AREJEE ATLETICO

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE
HABARI

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA
HABARI

MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
Legal Manager / Company Secretary Job Vacancy at BRAC Tanzania Finance LTD
HABARI

Legal Manager / Company Secretary Job Vacancy at BRAC Tanzania Finance LTD

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
5 Various Job Vacancies at Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)
HABARI

5 Various Job Vacancies at Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
Digital Channels Manager Job Vacancy at Airtel Tanzania PLC
HABARI

Digital Channels Manager Job Vacancy at Airtel Tanzania PLC

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
July 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
« Jun   Aug »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In