ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, August 13, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NMB YATOA VIFAA VYA AFYA NA ELIMU WILAYA YA LUSHOTO

I am Krantz by I am Krantz
Jul 14, 2022
in HABARI
0
NMB YATOA VIFAA VYA AFYA NA ELIMU WILAYA YA LUSHOTO
0
SHARES
54
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Benki ya NMB imetoa msaada wa mabati 200 kwa Zahanati ya Kwemakame iliyopo wilayani Lushoto mkoani Tanga yenye thamani ya Sh. milioni 7.1 na madawati 50 katika Shule ya Msingi Mbula B iliyopo wilayani humo yenye thamani ya Sh.milioni 3.9 ambapo jumla ya msaada huo ni Sh. milioni 11.

RelatedPosts

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

Aug 13, 2022

Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022

Aug 12, 2022

BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji

Aug 12, 2022
Load More

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper alisema kuwa benki hiyo inatambua juhudi za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Samia Suluhu Hassan za kusimamia huduma za afya na elimu kwa nguvu zote kwa kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma hizo mjini na vijijini.

Meneja huyo wa kanda alisema walipopata maombi ya kuchangia katika maendeleo ya elimu kwa Wilaya ya Lushoto walifarijika na kushirikiana nao ili ikawe chachu ya maendeleo ya sekta ya afya na elimu kwa jamii yao hasa katika zahanati ya Kwemakame na kwa Shule ya Msingi Mbula B.

Aliongeza kuwa imani yao ni kuwa vifaa hivyo vitatumika vyema kwa manufaa makubwa ya wananchi wa wilaya hiyo. ” Vifaa vinavyokwenda shuleni basi watoto wetu na wadogo zetu watakwenda kunufaika vyema kabisa na hata kusaidia ufaulu wao.,” alisema na kuongeza:

 

 

 

 

“Benki ya NMB tumekuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii, ni kwa zaidi ya miaka saba mfululizo tumekuwa tukitenga asilimia 1% ya faida yetu kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayotuzunguka, “alibainisha Prosper.

Awali akipokea msaada huo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Kalist Lazaro aliishukuru benki hiyo kwa msaada huo na kueleza kuwa msaada huo wa madawati unakwenda kuwatoa watoto wao kwenye vumbi na hatimaye sasa kukaa kwenye madawati huku mabati hayo yakienda kusaidia kwenye huduma za afya.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Ikupa Mwasioge alisema benki hiyo imekuwa ikijihusisha na utoaji wa misaada katika jamii zao kwani mbali na msaada huo hivi karibuni waliwapatia msaada wa vifaa katika kituo cha afya cha Mlalo.

Mjumbe wa kamati ya shule hiyo alisema kwa niaba ya kamati ya shule na wazazi wa kijiji hicho wameishukuru benki ya NMB kwa kuwapatia msaada huo ambao unakwenda kuongeza ufaulu shuleni hapo.

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

“Haya mabati 200 yanakwenda kutusaidia katika Zahanati yetu ya Kwemakame kuezeka kwani ilijengwa na bado haijaezekwa mabati, “alisema William Aloyce – Mtendaji wa Kijiji cha Kwemakame Kata ya Kwai.

MWISHO

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene
BIASHARA

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

by I am Krantz
Aug 13, 2022
Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022
HABARI

Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji
HABARI

BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini
HABARI

Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.
BIASHARA

Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.

by I am Krantz
Aug 12, 2022
Rais Samia Akamilisha Ziara yake Mkoani Njombe
HABARI

Rais Samia Akamilisha Ziara yake Mkoani Njombe

by ALFRED MTEWELE
Aug 11, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
July 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
« Jun   Aug »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In