ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, August 13, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO

I am Krantz by I am Krantz
Jul 3, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO
0
SHARES
51
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

NA
MWANDISHI WETU, SABASABA

WAJASIRIAMALI
wadogo na wa Kati wanayo nafasi kubwa ya kujenga maisha yao ya sasa na ya baadaye
kwa kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii NSSF, Meneja wa Sekta Isiyo
Rasmi wa Mfuko huo, Bi. Rehema Chuma  (pichani juu), amesema.

RelatedPosts

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

Aug 13, 2022

Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022

Aug 12, 2022

BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji

Aug 12, 2022
Load More

Amesema
chini ya Mpango wa Kitaifa wa Hifadhi ya Jamii kwa Sekta Isiyo Rasmi, ni muhimu
kundi hilo nalo liingie kwenye Hifadhi ya Jamii ili na wao wanapofika umri
ambao hautawawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali waweze kufaidika na
Mafao ambayo wenzao waliokuwa kwenye sekta rasmi (ajira rasmi) wanayapata.

Amewataja
Wajasiriamai hao walio katika sekta isiyo rasmi kuwa ni wote wanaofanya
shughuli za kuwapatia kipato halali na kutolea mfano, Bodaboda, Mamalishe, Machinga,
Waendesha bajaji, Mafundi cherehani, Wakaanga chipsi, Saluni za kike na kiume
na Mafundi Uashi.

“Tunaposema
tunajenga Maisha yako ya Sasa na  ya Baadaye,
mwanachama atafaidika kwa kupata Mafao mbalimbali mathalan tuna Fao la Uzazi
hili litamuhusisha mwana mama ambaye alikuwa mjamzito, Fao la Msaada wa Mazishi
na Fao la Mirathi, lakini tuna Fao la Uzee ambalo hili ndio fao muhimu kwa mtu
ambaye uwezo wa kufanya kazi umekoma, mfano kwa uzee au maradhi,”alifafanua.

Meneja
huyo ambaye alikuwa akiwahamasisha wananchi wanaotembelea Maonesho ya 46 ya
Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam kwenye viwanja vya Julius Nyerere
maarufu Sabasaba kujiunga na Mfuko huo, Julai 2, 2022, amesema ni rahisi sana
kujiunga.

“Mwanachama
anaweza kujiunga kwenye ofisi zetu zilizoenea kote nchini na kwa wale
wanaotembelea Maonesho haya ya Sabasaba tuko banda namba 13, njoo na kitambulisho
cha NIDA au Namba, kisha utajaza fomu na kupigwa picha, na papo hapo tutakutengenezea
kitambulisho na kuwa mwanachama rasmi wa NSSF.” Alifafanua na kuongeza hata kama
mtu hana kitambulisho cha NIDA, bado anaweza kuandikishwa.

Kuhusu
viwango vya uchangiaji Meneja huyo alisema kima cha chini cha uchangianji kila
mwezi ni shilingi elfu ishirini (20,000/=) lakini anaweza kuchangia zaidi
kulingana na kipato chake.

Aidha
alisema baada ya mwanachama kupata kitambulisho chake na namba ya uanachama,
uwasilishaji michango nao pia ni rahisi,

“Sasa
hivi mfumo wa kulipa kupitia simu ndio umezoeleka sana na sisi tunatumia
utaratibu huo wa kufanya malipo ya serikali kupitia mitandao ya simu, benki au
wakala wa benki.” Alifafanua.

Aliwaondoa
hofu wajasiriamali hao kuwa hata kama kipato chake wakati mwingine
hakimuwezeshi kulipa shilingi elfu 20 kwa mkupuo, anaweza kuchangia kidogo
kidogo kama shilingi elfu 2,000/=, 5,000/= na kuendelea kupitia namba maalum ya
malipo aliyopewa (control Number) ilimradi inapotimia mwezi mwanachama awe
amekamilisha malipo ya shilingi elfu 20,000/= kwasababu Mfumo unatambua kiwango
hicho cha chini cha uchangiaji kwa mwezi.

Meneja wa Sekta Isiyo Rasmi wa Mfuko huo, Bi. Rehema Chuma amesema (katikati), akimpatia elimu na kujibu mwaswali kutoka kwa mjasiriamali huyu (kulia) aliyetembelea banda la Mfuko huo Julai 2, 2022.

Bi. Rehema Chuma (kulia), akibadilishana mawazo na Meneja wa NSSF Mkoa wa Temeke Bw. Feruzi Mtika kwenye banda la Mfuko huo Julai 2, 2022

Afisa Matekelezo Mwandamizi, NSSF, Bi. Ummy Kimario (kulia), akimuhudumia mwananchi aliyefika kwenye banda la NSSF.

 Afisa Matekelezo Mkuu, NSSF, Bi. Asha Salum (kushoto), akimsikliza mwanachama wa Mfuko huo aliyetembelea banda la NSSF ili kuhudumiwa

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene
BIASHARA

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

by I am Krantz
Aug 13, 2022
Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022
HABARI

Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji
HABARI

BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini
HABARI

Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
STAMICO YAADHIMISHA MIAKA 50 TANGU IANZISHE
BIASHARA

STAMICO YAADHIMISHA MIAKA 50 TANGU IANZISHE

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.
BIASHARA

Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.

by I am Krantz
Aug 12, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
July 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
« Jun   Aug »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In