ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Monday, March 20, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

WAZIRI MBARAWA AWATAKA WAKANDARASI NA WAZABUNI KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEZESHAJI KUTOKA BENKI YA CRDB

I am Krantz by I am Krantz
Jul 21, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
WAZIRI MBARAWA AWATAKA WAKANDARASI NA WAZABUNI KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEZESHAJI KUTOKA BENKI YA CRDB
0
SHARES
157
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
 

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amewataka wakandarasi na wazabuni nchini kutumia fursa za uwezeshaji zinazotolewa na Benki ya CRDB ili kuongeza ufanisi katika kazi zao, na kuwajengea uwezo wa kushiriki kikamilifu katika miradi ya kimkakati nchini.

Prof. Mbalawa alisema hayo wakati akifungua Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni lililoandaliwa na Benki ya CRDB katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam. Mheshimiwa Waziri alisema fursa hizo zitasaidia kupunguza changamoto za ucheleweshwaji wa miradi mbalimbali kwasababu ya kukosekana kwa mtaji.

RelatedPosts

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA BENKI YA CRDB, AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA BENKI YA CRDB, AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA

Aug 9, 2022

BENKI YA CRDB YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE KITAIFA, JIJINI MBEYA

Aug 2, 2022

Benki Ya CRDB Na IFC Kuongeza Upatikanaji Wa Mitaji Kwa Wajasiriamali Nchini Tanzania Na Burundi

Jul 12, 2022
Load More

“Benki ya CRDB imewaletea fursa mlangoni, itumieni kupata mitaji nafuu kujijengea uwezo utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika miradi,” alisema Prof. Mbarawa huku akibainisha kuwa uwezeshaji huu unaofanywa na Benki ya CRDB utasidia kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha wakandarasi wazawa wanashiriki katika miradi (local content).

Prof. Mbalawa alipongeza Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali katika miradi ya ujenzi wa miondombinu mbalimbali nchini ambayo itasadia kuchochea ukuaji wa uchumi. “Tunatambua na kuthamini sana ushikiri wa Benki ya CRDB katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati nchini, asanteni na hongereni sana,” alisema.

ADVERTISEMENT

Prof. Mbalawa aliishauri Benki ya CRDB kupunguza riba katika mikopo ya wakandarasi kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa sekta nyengine ikiwamo ya kilimo ili kuwajengea uwezo wakandarasi na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika miradi inayotekelezwa na Serikali.

“Tunawapongeza kwa mikopo hii isiyo na dhamana na maboresho mengine mliyofanya, lakini niwaombe mpunguze riba ili kutoa unafuu zaidi. Vilevile, nitoe rai kwa Wakandarasi kurejesha mikopo kwa wakati kama ilivyo katika makubaliano,” aliongezea Prof. Mbalawa huku akiishauri Benki ya CRDB kuisaidia Serikali kutoa mafunzo ya usimamizi wa miradi kwa Wakandarasi na Wazabuni.

Aidha, Prof. Mbarawa alipongeza uamuzi wa Benki ya CRDB kufungua kampuni tanzu katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) akisema uamuzi huo utasaidia kufungua fursa nyingi kwa wafanyabiashara nchini ikiwamo wakandarasi na wazabuni.

“Congo kuna uhitaji mkubwa wa miundombinu ya barabara na nchi zetu zimekuwa katika mazungumzo ya namna gani tunaweza kusaidia katika kuboresha eneo hili hasa ukizingatia biashara baina ya nchi zetu inaendelea kukua”, alisema Prof. Mbalawa huku akihitimisha kwa kuipongeza Benki hiyo kwa kutunikiwa tuzo ya Benki Bora Tanzania na jarida la Euromoney la nchini Uingereza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alimhakikishia Prof. Mbalawa kuwa Benki ya CRDB kupitia kauli mbiu yake ya “Tupo Tayari” imejipanga vilivyo katika kuhakikisha inashirikiana na Serikali kuboresha miundombinu nchini ili kufungua fursa za kiuchumi na kuvutia wawekezaji.

Nsekela alisema Benki ya CRDB imefanya maboresho katika huduma zake inazotoa kwa kundi hilo ambapo hivi sasa wakandarasi wakubwa na wadogo watawezeshwa kupata huduma za mikopo bila dhamana yoyote. Alisema baadhi ya huduma zilizofanyiwa maboresho ni pamoja na dhamana ya zabuni “Bid bond”, dhamana za utekelezaji wa miradi “Performance Guarantee”, dhamana za malipo ya awali “Advance Payment Guarantee”, pamoja na huduma za mikopo ya mitambo.

Nsekela aliongezea kuwa Benki hiyo pia imeboresha taratibu zake za utoaji mikopo na hivyo kuwasihi Wakandarasi kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo, kufungua akaunti, pamoja na kujiunga na huduma za bima ili kujikinga na majanga yanayoweza kutokea. “Benki ya CRDB ni Benki yenu, niwahakikishie tu sisi Tupo Tayari kuwahudumia,” alihitimisha Nsekela.

Akizungumza kwa niaba ya wakandarasi na wazabuni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya ukandarasi ya Gopa Contractors Tanzania Ltd, Godfrey Mogellah aliipongeza Benki ya CRDB kwa hatua hiyo ya kuwakutanisha wadau wa sekta ya ujenzi nchini huku akieleza fursa zinazotolewa na Benki ya CRDB zitakwenda kuleta sura mpya katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa akizungumza katika Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni nchini lililoandaliwa na Benki ya CRDB leo tarehe 21 Julai 2022 katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.

Afisa Mkuu wa Biashara Benki ya CRDB, Boma Raballa akizungumza katika Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni nchini lililoandaliwa na Benki ya CRDB leo tarehe 21 Julai 2022 katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Kingo cha Biashara wa Benki ya CRDB, Toyi Ruvumbagu akizungumza katika Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni nchini lililoandaliwa na Benki ya CRDB leo tarehe 21 Julai 2022 katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya wakandarasi na wazabuni waliohudhuria Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni nchini lililoandaliwa na Benki ya CRDB wakifatilia mada mbalimbali leo tarehe 21 Julai 2022 katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wapili kulia), Afisa Mkuu wa Fedha Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo (kulia), Afisa Mkuu wa Biashara Benki ya CRDB, Boma Raballa (wapili kushoto), na Afisa Mkuu wa Uendeshaji Benki ya CRDB, Bruce Mwile, wakiwa pamoja na baadhi ya wakandarasi na wazabuni waliohudhuria Kongamano la Uwezeshaji kwa Wakandarasi na Wazabuni nchini lililoandaliwa na Benki ya CRDB leo tarehe 21 Julai 2022 katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.

ADVERTISEMENT

Related

Tags: CRDB
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

RJ THE DJ VIFO VINAONGEZA MSONGO WA MAWAZO
HABARI

ROMY JONS AOMBA MSAMAHA

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
MCHUNGAJI AFUNGA KANISA KISA ASHINDA MIL 100 ZA “KUBETI”
HABARI

MCHUNGAJI AFUNGA KANISA KISA ASHINDA MIL 100 ZA “KUBETI”

by ALFRED MTEWELE
Mar 20, 2023
WAZIRI BITEKO ATAKA BAJETI YA 2023/24 KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA
HABARI

WAZIRI BITEKO ATAKA BAJETI YA 2023/24 KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
TMA YATOA TAHADHARI MVUA KUBWA MIKOA HII KUANZIA LEO NA KESHO
HABARI

TMA YATOA TAHADHARI MVUA KUBWA MIKOA HII KUANZIA LEO NA KESHO

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
WATU 5 WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA WIZI MAFUTA SGR
HABARI

WATU 5 WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA WIZI MAFUTA SGR

by ALFRED MTEWELE
Mar 20, 2023
MARUFUKU KUTOA FEDHA UPATE DHAMANA POLISI
HABARI

MARUFUKU KUTOA FEDHA UPATE DHAMANA POLISI

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
July 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
« Jun   Aug »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In