Mkurugenzi Mkuu wa Pesapal Tanzania, Bupe Mwakalundwa (kushoto), akipokea leseni iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa ajili ya kufanya biashara ya kutoa huduma kwa mifumo ya malipo ya kidijitali kutoka kwa Meneja Msimamizi wa Wateja wa kampuni hiyo, Ally Abdul. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Kampuni ya Pesapal Tanzania imepewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kufanya biashara nchini kama mtoa huduma wa mifumo ya malipo ya kidijitali.
Pesapal ambayo ni taasisi ya teknolojia za huduma za kifedha (fintech) imesema jana kuwa imepewa idhini hiyo chini ya sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa ya Mwaka 2015.
Tayari Pesapal inafanya biashara Kenya na Uganda ambako inazihudumia zaidi ya biashara ndogo na za kati 50,000. Dira yake ni kuziwezesha nchi za Kiafrika kutoa huduma za kifedha za kidijitali zenye bei nafuu, salama na zinazozingatia mahitaji ya soko husika kwa ajili ya kuchochea ukuaji uchumi endelevu.
Maafisa wake waandamizi wamesema hivyo ndivyo kampuni hiyo itakavyofanya Tanzania baada ya kupata leseni ya BoT ambapo kimsingi ni kutoa huduma ya malipo mtandaoni na kusaidia kufanyika malipo kwa ufanisi.
“Kuweza kupenya na kupanua shughuli zake nchini Tanzania ni hatua kubwa ya kimkakati yenye tija kwa Pesapal, ambayo ina matarajio ya kufanya vizuri sokoni na kuwawezesha Watanzania kupata thamani kutoka kwenye suluhisho za kifedha bunifu za kidijitali zilizosalama na zenye manufaa makubwa,” kampuni hiyo ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari.
Katikati ya mwaka jana, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliipa baraka kampuni hiyo kufanya biashara nchini ambazo ni muhimu kabla ya kukubaliwa kufanya hivyo na Benki Kuu.
Akizungumzia kupatikana kwa leseni hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Pesapal Tanzania, Bi Bupe Mwakalundwa, alisema kupatikana kwa leseni hiyo kutaiwezesha kampuni yao kupanua wigo wa upatikanaji wa bidhaa zao barani Afrika.
Kama ilivyo BoT, alifafanua, Pesapal ni muumini wa matumuzi ya teknolojia kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya huduma jumuishi za kifedha.
“Kwetu sisi Pesapal, lengo letu ni kuimarisha teknolojia ili kutengeneza suluhisho za malipo zinazorahisisha jinsi wateja na baishara mbalimbali wanavyolipwa,” alisema.
Bi Bupe aliongeza kuwa Pesapal inataka kuwapa Watanzania fursa ya kupata huduma bunifu za kifedha na kidijitali ambazo zinafaa kwa kada na biashara zote.
Wanufaika wengine wa uwekezaji huo watakuwa ni wafanyabiashara wa mtandaoni, watu binafsi, na wale wote ambao kwa sasa hawajafikiwa na mifumo rasmi ya kawaida ya malipo.
Kwa mujibu wa Afisa Mtendaji Mkuu na Mwanzilishi wa Pesapal Group, Agosta Liko, kampuni hiyo imekuwa kinara wa fedha kidijitali katika ukanda huu wa Afrika Mashariki kwa kuchangia pakubwa uboresha wa huduma za malipo.
“Sisi kama kampuni ya kutoa huduma na iliyojikita zaidi kutumia teknolojia kwenye uendeshaji na uzalishaji wake tunazo zana hitajika kuleta mabadiliko katika upatikanaji wa huduma za fedha kidijitali,” Bw Liko alinukuriwa kwenye taarifa ya Pesapal Tanzania kwa vyombo vya habari.
Alisema hilo litawezekana kwa wao kuja na suluhisho zinazozingatia huduma bora kwa wateja, kusaidia watu kuboresha matumizi ya fedha na kuzisaidia biashara kutatua changamoto zote zinazohusiana na malipo.
Pesapal ilianzishwa mwaka 2009 lengo lake kuu likiwa ni kuchangia kusaidia kurahisisha kulipana na katika miaka 11 iliyopita imefanikiwa katika hilo kwa kiasi kikubwa kutokana na uwekezaji ambao imekuwa inafanya.
MWISHO…
****
Pesapal secures BoT licence to operate in Tanzania
By A Special Correspondent
The central bank has granted Pesapal Tanzania a licence to operate in the local digital financial services space as a payment systems provider (PSP), the company said yesterday.
In a statement announcing the payment solutions development, the financial technology (fintech) firm said the Bank of Tanzania (BoT) has licensed it under the National Payment System Act of 2015.
Already Pesapal operates in Kenya and Uganda where it serves over 50,000 general enterprises. The vision of the company is to empower Africa to access affordable, convenient, secure and innovative digital financial services that spur sustainable growth.
Its senior officials said the BoT licence allows it to do exactly that in Tanzania, which principally is providing online and point-of-sale payments seamlessly.
“Penetrating and expanding its operations in Tanzania is a beneficial strategic move for Pesapal, which hopes to gain a foothold in the market, and enable Tanzanians to derive value from access to innovative, secure, and economical digital financial solutions,” Pesapal Tanzania noted in the presser.
Mid last year, Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) blessed its quest to do business in the country which was a key aspect for the acquisition of the BoT licence.
Commenting on the development, Ms Bupe Mwakalundwa, Pesapal Tanzania Country Manager, said obtaining the PSP licence enables the company to broaden its product portfolio and market outreach in Africa.
Like BoT, Ms Bupe explained, Pesapal believes in technology being a key driver for economic growth and supporting financial inclusion for all.
“At Pesapal, our goal is to leverage technology to build payment solutions that simplify how consumers and businesses get paid,” she pointed out.
Through the venture, she added, Pesapal wants to provide Tanzanians with access to innovative digital financial products that are suited for all enterprises across the board, including SMEs. Other beneficiaries of the investment will be online merchants, individuals, and all those currently underserved by traditional payment mechanisms.
According to Agosta Liko, Pesapal Group CEO and Founder, the company has become a champion of digital finance in the region by playing a major role in disrupting payments services for the better.
“As a service-oriented, product-driven, and technology-intensive organization, we have the tools to drive change in digital financial services. We will do this by providing solutions that ensure superior customer experience, help people streamline their financial lives, and continue to support businesses by solving the complexity of handling payments,” he noted in the statement.
Pesapal was founded in 2009 to make it easy for people and businesses to pay and get paid. In the last 11 years, the company has invested heavily in the business to build an innovative financial services ecosystem for businesses and consumers that is anchored by integrity and unmatched value.
Ends…