ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, June 2, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

Pesapal yapewa Leseni na Benki Kuu ya Tanzania kwa Utoaji Huduma Kwa Mfumo wa Kidigitali Zaidi

Dar es Salaam, Tanzania

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Aug 17, 2022
in BIASHARA
0
Pesapal yapewa Leseni na Benki Kuu ya Tanzania kwa Utoaji Huduma Kwa Mfumo wa Kidigitali Zaidi
0
SHARES
140
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mkurugenzi Mkuu wa Pesapal Tanzania, Bupe Mwakalundwa (kushoto), akipokea leseni iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa ajili ya kufanya biashara ya kutoa huduma kwa mifumo ya malipo ya kidijitali kutoka kwa Meneja Msimamizi wa Wateja wa kampuni hiyo, Ally Abdul. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.

RelatedPosts

No Content Available
Load More

Kampuni ya Pesapal Tanzania imepewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kufanya biashara nchini kama mtoa huduma wa mifumo ya malipo ya kidijitali.

Pesapal ambayo ni taasisi ya teknolojia za huduma za kifedha (fintech) imesema jana kuwa imepewa idhini hiyo chini ya sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa ya Mwaka 2015.

Tayari Pesapal inafanya biashara Kenya na Uganda ambako inazihudumia zaidi ya biashara ndogo na za kati 50,000. Dira yake ni kuziwezesha nchi za Kiafrika kutoa huduma za kifedha za kidijitali zenye bei nafuu, salama na zinazozingatia mahitaji ya soko husika kwa ajili ya kuchochea ukuaji uchumi endelevu.

Maafisa wake waandamizi wamesema hivyo ndivyo kampuni hiyo itakavyofanya Tanzania baada ya kupata leseni ya BoT ambapo kimsingi ni kutoa huduma ya malipo mtandaoni na kusaidia kufanyika malipo kwa ufanisi.

“Kuweza kupenya na kupanua shughuli zake nchini Tanzania ni hatua kubwa ya kimkakati yenye tija kwa Pesapal, ambayo ina matarajio ya kufanya vizuri sokoni na kuwawezesha Watanzania kupata thamani kutoka kwenye suluhisho za kifedha bunifu za kidijitali zilizosalama na zenye manufaa makubwa,” kampuni hiyo ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari.

Katikati ya mwaka jana, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliipa baraka kampuni hiyo kufanya biashara nchini ambazo ni muhimu kabla ya kukubaliwa kufanya hivyo na Benki Kuu.

Akizungumzia kupatikana kwa leseni hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Pesapal Tanzania, Bi Bupe Mwakalundwa, alisema kupatikana kwa leseni hiyo kutaiwezesha kampuni yao kupanua wigo wa upatikanaji wa bidhaa zao barani Afrika.

Kama ilivyo BoT, alifafanua, Pesapal ni muumini wa matumuzi ya teknolojia kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya huduma jumuishi za kifedha.

“Kwetu sisi Pesapal, lengo letu ni kuimarisha teknolojia ili kutengeneza suluhisho za malipo zinazorahisisha jinsi wateja na baishara mbalimbali wanavyolipwa,” alisema.

Bi Bupe aliongeza kuwa Pesapal inataka kuwapa Watanzania fursa ya kupata huduma bunifu za kifedha na kidijitali ambazo zinafaa kwa kada na biashara zote.

Wanufaika wengine wa uwekezaji huo watakuwa ni wafanyabiashara wa mtandaoni, watu binafsi, na wale wote ambao kwa sasa hawajafikiwa na mifumo rasmi ya kawaida ya malipo.

Kwa mujibu wa Afisa Mtendaji Mkuu na Mwanzilishi wa Pesapal Group, Agosta Liko, kampuni hiyo imekuwa kinara wa fedha kidijitali katika ukanda huu wa Afrika Mashariki kwa kuchangia pakubwa uboresha wa huduma za malipo.

“Sisi kama kampuni ya kutoa huduma na iliyojikita zaidi kutumia teknolojia kwenye uendeshaji na uzalishaji wake tunazo zana hitajika kuleta mabadiliko katika upatikanaji wa huduma za fedha kidijitali,” Bw Liko alinukuriwa kwenye taarifa ya Pesapal Tanzania kwa vyombo vya habari.

Alisema hilo litawezekana kwa wao kuja na suluhisho zinazozingatia huduma bora kwa wateja, kusaidia watu kuboresha matumizi ya fedha na kuzisaidia biashara kutatua changamoto zote zinazohusiana na malipo.

Pesapal ilianzishwa mwaka 2009 lengo lake kuu likiwa ni kuchangia kusaidia kurahisisha kulipana na katika miaka 11 iliyopita imefanikiwa katika hilo kwa kiasi kikubwa kutokana na uwekezaji ambao imekuwa inafanya.

MWISHO…

****

Pesapal secures BoT licence to operate in Tanzania

By A Special Correspondent

ADVERTISEMENT

The central bank has granted Pesapal Tanzania a licence to operate in the local digital financial services space as a payment systems provider (PSP), the company said yesterday.

In a statement announcing the payment solutions development, the financial technology (fintech) firm said the Bank of Tanzania (BoT) has licensed it under the National Payment System Act of 2015.

Already Pesapal operates in Kenya and Uganda where it serves over 50,000 general enterprises. The vision of the company is to empower Africa to access affordable, convenient, secure and innovative digital financial services that spur sustainable growth.

Its senior officials said the BoT licence allows it to do exactly that in Tanzania, which principally is providing online and point-of-sale payments seamlessly.

“Penetrating and expanding its operations in Tanzania is a beneficial strategic move for Pesapal, which hopes to gain a foothold in the market, and enable Tanzanians to derive value from access to innovative, secure, and economical digital financial solutions,” Pesapal Tanzania noted in the presser.

Mid last year, Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) blessed its quest to do business in the country which was a key aspect for the acquisition of the BoT licence.

Commenting on the development, Ms Bupe Mwakalundwa, Pesapal Tanzania Country Manager, said obtaining the PSP licence enables the company to broaden its product portfolio and market outreach in Africa.

Like BoT, Ms Bupe explained, Pesapal believes in technology being a key driver for economic growth and supporting financial inclusion for all.

“At Pesapal, our goal is to leverage technology to build payment solutions that simplify how consumers and businesses get paid,” she pointed out.

ADVERTISEMENT

Through the venture, she added, Pesapal wants to provide Tanzanians with access to innovative digital financial products that are suited for all enterprises across the board, including SMEs. Other beneficiaries of the investment will be online merchants, individuals, and all those currently underserved by traditional payment mechanisms.

According to Agosta Liko, Pesapal Group CEO and Founder, the company has become a champion of digital finance in the region by playing a major role in disrupting payments services for the better.

“As a service-oriented, product-driven, and technology-intensive organization, we have the tools to drive change in digital financial services. We will do this by providing solutions that ensure superior customer experience, help people streamline their financial lives, and continue to support businesses by solving the complexity of handling payments,” he noted in the statement.

Pesapal was founded in 2009 to make it easy for people and businesses to pay and get paid. In the last 11 years, the company has invested heavily in the business to build an innovative financial services ecosystem for businesses and consumers that is anchored by integrity and unmatched value.

Ends…

Related

Tags: pesapal tanzania
ADVERTISEMENT
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

VODACOM IMEZINDUA RASMI SIMU AINA YA TECNO CAMON 20 SERIES YENYE UWEZO WA 5G
BIASHARA

VODACOM IMEZINDUA RASMI SIMU AINA YA TECNO CAMON 20 SERIES YENYE UWEZO WA 5G

by ALFRED MTEWELE
May 23, 2023
BENKI YA NBC YAKABIDHI GAWIO LA TSH. BIL 20 KWA WANAHISA WAKE, YAJIVUNIA MAFANIKIO
BIASHARA

BENKI YA NBC YAKABIDHI GAWIO LA TSH. BIL 20 KWA WANAHISA WAKE, YAJIVUNIA MAFANIKIO

by ALFRED MTEWELE
May 17, 2023
KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO TAREHE 17 MEI  2023
BIASHARA

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO TAREHE 17 MEI 2023

by I am Krantz
May 17, 2023
KUTOKA KURASA ZA Magazetiya Tanzania leo MEI 14, 2023
BIASHARA

KUTOKA KURASA ZA Magazetiya Tanzania leo MEI 14, 2023

by I am Krantz
May 14, 2023
BENKI YA CRDB YAZINDUA MIKOPO YA HIJA NA UMRAH ISIYO NA RIBA
BIASHARA

BENKI YA CRDB YAZINDUA MIKOPO YA HIJA NA UMRAH ISIYO NA RIBA

by ALFRED MTEWELE
May 11, 2023
KUTOKA KATIKA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 11 MEI 2023    #KoncepttvUpdates
BIASHARA

KUTOKA KATIKA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 11 MEI 2023 #KoncepttvUpdates

by I am Krantz
May 11, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
August 2022
M T W T F S S
1234567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In