ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT
RIPOTI kutoka Ubelgiji zinamhusisha mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ‘Samagoal’ kutua Cardiff City ya Ligi Daraja la Kwanza England ‘Championship’.
–
Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 29 ameonyeshewa malango wa kutokea huko Uturuki kwenye klabu yake ya Fenerbahce baada ya kutokuwa kwenye mipango ya kocha mpya wa kikosi hicho, Jorge Jesus, raia wa Ureno.
–
Mwandishi wa habari wa Ubelgiji, Sacha Tavolieri ameripoti kuwa Cardiff wapo kwenye mazungumzo juu ya uwezekano wa kumchukua mshambuliaji huyo kwa mkopo.
–
Credit : Mwanaspoti