ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, August 13, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Ufadhili wa NMB wafikia Sh. trilioni 1.56 sekta ya kilimo

I am Krantz by I am Krantz
Aug 3, 2022
in HABARI
0
Ufadhili wa NMB wafikia Sh. trilioni 1.56 sekta ya kilimo
0
SHARES
21
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Meneja wa NMB Nyanda ya Juu, Straton Chilongola akimkabidhi risala kuhusu utendaji wa NMB kwenye Sekta ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango katika ufunguzi rasmi wa maonesho ya NaneNane mjini Mbeya.

 

RelatedPosts

NMB yaahidi kuendeleza kunufaisha sekta ya kilimo nchini

NMB yaahidi kuendeleza kunufaisha sekta ya kilimo nchini

Aug 10, 2022

NMB Yaibuka Kinara tena Utoaji Huduma Bora Nanenane 2022

Aug 9, 2022

Benki Ya NMB Yaendelea Kuwa Kinara Wa Ufanisi Nchini Tanzania

Jul 29, 2022
Load More

 

Serikali imezichangisha benki nchini kwa lengo la kuongeza wigo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kukopa ili kuongeza uwekezaji kwenye sekta ya kilimo ili waweze kuchangia zaidi juhudi za ujenzi wa Taifa.

Akizungumza kwenye ufunguzi rasmi wa maonyesho ya Nanenane 2022 yanayofanyika Kitaifa mkoani Mbeya, Makamu wa Rais,Dk. Philip Mpango, alizitaka taasisi za fedha kuchangia zaidi shughuli za kilimo cha mazao,ufugaji na uvuvi.

ADVERTISEMENT

Kwa mujibu wa Dk. Mpango, wakulima, wafugaji na wavuvi wanahitaji mikopo zaidi ili kuongeza uwekezaji na uzalishaji kwa ajili ya kupunguza changamoto ya ajira nchini.

Aliendelea kueleza kuwa maendeleo ya kilimo yanahitaji ufadhili mkubwa kitu ambacho Benki ya NMB imesema imekuwa ikifanya kwa muda mrefu na kuwekeza zaidi ya Shilingi trilioni 1.56 katika miaka mitano iliyopita.

Akizungumzia mikopo hiyo, Meneja wa NMB Nyanda za Juu,Straton Chilongola, alisema ukopeshaji unaofanywa na benki hiyo umekuwa na tija kubwa katika mnyororo wa thamani wa kilimo nchini.

“Mikopo ya NMB imewawezesha wakulima, wavuvi na wafugaji kuchangia ukuaji wa pato la taifa na maendeleo ya nchi kwa ujumla.” alisema Chilongola

Akielezea ufadhili wa NMB kwenye sekta hiyo, alisema mikopo ambayo imetolewa na benki hiyo ni pamoja na zaidi ya Shilingi bilioni 300 mwaka huu kwa ajili ya kilimo cha kahawa, tumbaku, parachichi, mpunga, ufuta, soya na mahindi na Shilingi bilioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa maghala.

Pia, kupitia NMB Foundation, benki hiyo imetoa elimu ya fedha na mafunzo ya biashara kwa vyama vya ushirika wa wakulima (AMCOS) 1,550 nchi nzima, ili kuwajengea uwezo wa namna bora ya kusimamia mapato yao.

Kubwa zaidi, Benki ya NMB imekuja na Suluhisho kwenye masuala ya utatuzi wa kifedha kwa kuja na NMB Mshiko Fasta ambapo mkulima kupitia simu yake ya mkononi, anaweza kupata mkopo wa hadi 500,000 papo hapo bila dhamana akiwa na NMB Mkononi.

ADVERTISEMENT

MWISHO

Related

Tags: NMB
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene
BIASHARA

Mkazi wa Mufindi -Iringa akabidhiwa gari mpya Suzuki S Presso baada ya kuibuka mshindi promosheni ya Vodacom Tusua Mapene

by I am Krantz
Aug 13, 2022
Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022
HABARI

Rais Samia Akiwa katika Ziara yake Mkoani Iringa 2022

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji
HABARI

BIL.11 kupelekwa Mafinga kuboresha miundombinu ya Mji

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini
HABARI

Dkt. Mpango Aitaka NEMC na STAMICO Kufanya Tathimini Migodini

by ALFRED MTEWELE
Aug 12, 2022
Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.
BIASHARA

Benki ya NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane Mkoani Mbeya.

by I am Krantz
Aug 12, 2022
Rais Samia Akamilisha Ziara yake Mkoani Njombe
HABARI

Rais Samia Akamilisha Ziara yake Mkoani Njombe

by ALFRED MTEWELE
Aug 11, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
August 2022
M T W T F S S
1234567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293031  
« Jul    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In