ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, December 1, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Zawadi za Sh. Milioni 100 kushindaniwa CRDB Bank Marathon

I am Krantz by I am Krantz
Aug 2, 2022
in HABARI
0
Zawadi za Sh. Milioni 100 kushindaniwa CRDB Bank Marathon
0
SHARES
289
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

OTMI9605_1 

Ikiwa zimebaki siku 12 kuelekea msimu wa tatu wa CRDB Bank Marathon tarehe 14 Agosti 2022, imeelezwa kuwa jumla ya zawadi za shilingi milioni 100 zitashindaniwa katika mbio hizo zinazotarajiwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 6,000.

Taarifa hiyo imetolewa leo katika hafla fupi iliyokutanisha wadau na washirika wa CRDB Bank Marathon iliyofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.

OTMI9484

Akizungumza katika hafla hiyo, Nsekela amesema katika mbio za mwaka huu Benki hiyo imefanya maboresho makubwa katika zawadi ili kuongeza ushindani miongoni mwa washiriki, lakini pia kuendana na hadhi ya kimataifa ambayo mbio hizo ilipata mwaka jana.

“Katika mbio ndefu za 42.2km, washindi wa kwanza kwa upande wa wanaume na wanawake watapata shilingi milioni 10 kila mmoja. Washindi hawa pia watapata zawaidi ya kulala usiku mmoja hapa Johari Rotana, pamoja na vocha za zawadi katika duka la Justfit,” alieleza.

OTMI9246

Akitoa majumuisho ya zawadi hizo, Mkurugenzi wa Mawasiliano Benki ya CRDB, Tully Mwambapa alisema kuwa katika mbio hizo ikiwamo 21.1km, 10km, 5km, na baiskeli 65km washindi 6 wa kwanza watapewa zawadi za fedha taslimu.

Tully aliongezea pia kutakuwa na zawadi kwa makundi maalamu ya wazee, watoto, na wakimbiaji waliovaa kipekee. “Jumla ya zawadi hizi zote zitakazotolewa kwa washindi ni shilingi milioni 100,” alisema Tully.

OTMI9467

Katika hafla hiyo, Benki ya CRDB pia ilitambulisha vifaa vitakavyotumika katika msimu wa tatu wa CRDB Bank Marathon ikiwamo medali, fulana, kofia, bib, pamoja na mfuko wa kuwekea vifaa (back-pack), ambazo washiriki wa mbio hizo watapewa.

Kwa upande wa usajili, Nsekela alisema mpaka sasa tayari watu zaidi ya 4,200 tayari wameshajisajili kushiriki mbio hizo. Nsekela alibainisha kuwa kati yao 801 ni wakimbiaji kutoka nje ya nchi, na kutoa rai kwa Watanzania kuchangamkia nafasi zilizobaki.

“Niwashukuru wale wote waliojisajili katika mbio hizi. Kwa wale ambao bado niwasihi kutembelea tovuti yetu ya www.crdbbankmarathon.co.tz kujisajili, mtu binafsi atachangia shilingi 40,000 na washiriki kupitia vikundi ni shilingi 30,000,” alisema.

OTMI9296

Aliongezea: “Katika siku hizi chache zilizobaki tungependa zaidi kuona Watanzania wengi wakijitokeza kujisajili na kushiriki kwa wingi kwani hii ni marathon yetu na tungependa pia kuona zawadi hizi zikibaki nyumbani.”

Aidha Nsekela alitumia fursa hiyo kumshukuru Makamu, Dkt. Philip Mpango kwa kukubali kuwa mgeni rasmi kati mbio hizo. Aliongezea kuwa viongozi mbalimbali tayari wameshajisajili kushiriki ikiwamo Waziri wa Michezo, Mohamed Mchengerwa.

Viongozi wengine waliojisajili kushiriki ni Pamoja na Naibu Waziri wa Michezo, Pauline Gekule, Naibu Spika, Mussa Zungu, Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa,  Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, na Kati Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo.

OTMI9330

Akiongea kwa niaba ya washirika wa CRDB Bank Marathon, Mkurugenzi wa Mkuu wa Sanlam, Julius Magabe alisema kampuni yao inajivunia kuwa washirika wa CRDB Bank Marathon kutokana na mbio hizo kujikita zaidi katika kuhamasisha watu kusaidia jamii.

“Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuandaa mbio hizi zinazowaleta Watanzania kushiriki katika kutatua changamoto katika jamii. Sanlam ni kampuni ambayo inajali afya na mazingira ya watu wake hivyo tunakila sababu ya sisi kushiriki katika mbio hizi,” alisema Magabe.

OTMI9543

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuandaa mbio hizo ambazo zinalenga kukusanya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kusaidia gharama za matibabu kwa wakinamama wenye ujauzito hatarishi katika hospitali ya CCBRT, na upasuaji kwa watoto wenye matatizo ya moyo JKCI.

ADVERTISEMENT
OTMI9504

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi akitoa shukrani kwa Benki ya CRDB kwa kuandaa mbio hizo ambazo zinazolenga kukusanya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kusaidia gharama za matibabu kwa wakinamama wenye ujauzito hatarishi katika hospitali ya CCBRT, na upasuaji kwa watoto wenye matatizo ya moyo JKCI.

OTMI9579

 

OTMI9531
OTMI9632

 

OTMI9639

 

OTMI9644_1

 

OTMI9653

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Tuliishi maisha ya shida sana kisa uchawi wa jirani!
HABARI

Tuliishi maisha ya shida sana kisa uchawi wa jirani!

by I am Krantz
Nov 30, 2023
EACOP Yakamilisha Utaratibu Wa Fidia Kwa Kukabidhi Nyumba Ya 339 Mkoani Tanga
HABARI

EACOP Yakamilisha Utaratibu Wa Fidia Kwa Kukabidhi Nyumba Ya 339 Mkoani Tanga

by I am Krantz
Nov 29, 2023
MAWAKALA WA USAJILI WA VODACOM TANZANIA WATEMBELEA AFRIKA YA KUSINI KUTOKANA NA UTENDAJI BORA WA KAZI.
HABARI

MAWAKALA WA USAJILI WA VODACOM TANZANIA WATEMBELEA AFRIKA YA KUSINI KUTOKANA NA UTENDAJI BORA WA KAZI.

by I am Krantz
Nov 29, 2023
NMB, Oryx Tanzania wazindua ‘Moto Mkali Bei Poa,’ kukopesha gesi ya kupikia
HABARI

NMB, Oryx Tanzania wazindua ‘Moto Mkali Bei Poa,’ kukopesha gesi ya kupikia

by I am Krantz
Nov 27, 2023
Kampeni Ya Serengeti Maokoto Ndani Ya Kizibo Yazidi Kusambaza Furaha Kwa Watanzania
HABARI

Kampeni Ya Serengeti Maokoto Ndani Ya Kizibo Yazidi Kusambaza Furaha Kwa Watanzania

by I am Krantz
Nov 27, 2023
NMB Mlipa Kodi Mkubwa na Bora Zaidi Tanzania 2023 🇹🇿
HABARI

NMB Mlipa Kodi Mkubwa na Bora Zaidi Tanzania 2023 🇹🇿

by I am Krantz
Nov 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TWEETS

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
August 2022
M T W T F S S
1234567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In