ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, December 9, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Benki ya Stanbic yadhamiria kuwa chachu ya ushiriki wa wazawa katika uwekezaji nchini

I am Krantz by I am Krantz
Sep 22, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
Benki ya Stanbic yadhamiria kuwa chachu ya ushiriki wa wazawa katika uwekezaji nchini
0
SHARES
156
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Waziri Mkuu Mh Kasim Majaliwa akikabidhi cheti cha utambuzi wa udhamini wa benki ya Stanbic katika Kongamano la 6 la mwaka la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililoandaliwa na NEEC kwa Kai Mollel Mkuu wa Incubator.
Wafanyakazi wa benki ya Stanbic wakiwa katika Kongamano la 6 la mwaka la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililoandaliwa na NEEC hivi karibuni jijini Dodoma.
Mkuu wa Incubator wa benki ya Stanbic, Kai Mollel akizungumza wakati wa Kongamano la 6 la mwaka la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililoandaliwa na NEEC ambapo alitilia mkazo dhamira ya beknki hiyo kusaidia wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kutoa huduma zinazokidhi mahitaji yao na kutatua changamoto zinazowakabili.

Dar es Salaam, Septemba 21, 2022: Benki ya Stanbic Tanzania imetilia mkazo dhamira yake ya  kusaidia wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kutoa huduma zinazokidhi mahitaji yao na kutatua changamoto zinazowakabili. Ahadi hiyo ilitolewa na Mkuu wa Incubator wa Benki ya Stanbic, Kai Mollel, wakati wa Kongamano la 6 la mwaka la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lenye kaulimbiu: “Uwezeshaji wa Watanzania katika Uwekezaji’’ lililofanyika Septemba 19, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa LAPF, Dodoma huku benki hiyo ikiwa ndiyo mdhamini mkuu. 

 

Jukwaa hilo la siku moja lilihudhuriwa na Waziri Mkuu wa Muungano Jamhuri ya Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ambaye aliwapongeza wadhamini wakuu kwa kuisaidia NEEC kufanikisha jukwaa hili, huku akitilia mkazo kuwa  serikali inathamini mchango wao kwa kuzingatia kwamba serikali iko katika mpango wa kutengeneza mazingira mazuri ili watanzania waweze kushiriki katika shughuli za uwekezaji.

 

Wakati wa hotuba yake, Mollel aliahidi kuwa benki itafanya kazi bega kwa bega na serikali katika kusaidia ukuaji wa wajasiriamali. “Tunapenda kuihakikishia serikali, wafanyabiashara na wadau wote wa maendeleo kwamba sisi kama benki tutaendelea kushirikiana nanyi katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yetu.” Mollel alisema

 

Aidha aliipongeza NEEC kwa kuandaa kongamano hilo huku akiweka wazi kuwa benki hiyo imefurahi kuwa sehemu ya mazungumzo yatakayochochea uwekezaji wa ndani (Local content). “Benki yetu inaongoza kwa uwekezaji, na mwaka huu tumetunukiwa tuzo ya Benki Bora ya Uwekezaji na EuroMoney Market Leaders kwa mwaka 2022 kutoka kwa jarida la  EuroMoney. Hii ni kwa sababu tumeendelea kutoa huduma mbalimbali zinazowawezesha watanzania kushiriki na kunufaika na uwekezaji nchini.” alisema Mollel 

 

Benki ya Stanbic imekuwa katika safari ya ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati, na hivi karibuni imeingia ubia na NEEC kutekeleza programu ya Supplier Development ambapo wajasiriamali watapatiwa mafunzo na kupatiwa vitendea kazi vya kuwawezesha kutumia fursa za uwekezaji nchini na kuongeza ushindani wao kikanda na kimataifa.

 

Benki ya Stanbic inaendelea kupiga hatua katika kukuza uwekezaji miongoni mwa wateja wake nchini. Kuunga mkono jukwaa hili ni ishara kuwa benki imejidhatiti kuimarisha sekta ya uwekezaji, pamoja na kuwawezesha wananchi kutumia rasilimali na fursa zilizopo ili kuleta maendeleo ya kiuchumi katika taifa hili.

 

ADVERTISEMENT

End.

 

Related

Tags: stannic
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Legal Counsel Civil Litigation Job Vacancies at NMB Bank PLC – 2 Positions
BIASHARA

Legal Counsel Civil Litigation Job Vacancies at NMB Bank PLC – 2 Positions

by ALFRED MTEWELE
Dec 9, 2023
YALIYOJIRI KWENYE MAGAZETI YA LEO DESEMBA 9, 2023
HABARI

YALIYOJIRI KWENYE MAGAZETI YA LEO DESEMBA 9, 2023

by ALFRED MTEWELE
Dec 9, 2023
VIFO HANANG VYAFIKIA 80
HABARI

VIFO HANANG VYAFIKIA 80

by ALFRED MTEWELE
Dec 8, 2023
MVUA CHANZO KUKATIKA UMEME NCHINI
HABARI

MVUA CHANZO KUKATIKA UMEME NCHINI

by ALFRED MTEWELE
Dec 8, 2023
Marekani Yatoa Msaada Kukabiliana na Mafuriko nchini Tanzania
HABARI

Marekani Yatoa Msaada Kukabiliana na Mafuriko nchini Tanzania

by I am Krantz
Dec 8, 2023
MTOTO WA MIAKA 13 ALIYELAMBA DILI NONO KAMPUNI YA NIKE
BIASHARA

MTOTO WA MIAKA 13 ALIYELAMBA DILI NONO KAMPUNI YA NIKE

by ALFRED MTEWELE
Dec 8, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TWEETS

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
September 2022
M T W T F S S
 1234
567891011
12131415161718
19202122232425
2627282930  
« Aug   Oct »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In