Rais wa Equatorial Guinea, Teodoro Obiang Nguema Mbasogo ambaye ameiongoza nchi hiyo kwa miaka 43, amethibitisha kuwa atagombea tena katika uchaguzi wa Novemba.
–
Mtoto wake ambaye pia ni Makamu wa Rais, Teodoro Nguema Obiang Mangue, ametoa tangazo hilo kupitia ukurasa wa Twitter siku ya Ijumaa akisema ni “Kwa sababu ya haiba yake, uongozi wake na uzoefu wake wa kisiasa.”
ADVERTISEMENT
–
ADVERTISEMENT
Mashirika ya kutetea haki na mataifa ya kigeni yanasema kuwa utawala wa Obiang umekuwa na mateso kwa wapinzani wa kisiasa, wenye chaguzi za udanganyifu na ufisadi, lakini Obiang anakanusha mashtaka hayo.