WATU wengi wamezoea kuona mwanaume anamuoa mtu ambaye si damu yake yaani waliozaliwa na baba na mama mmoja, hii ni kutokana na maandiko ya vitabu vya dini na jamii nyingi huamini katika hilo.
–
Lakini imekuwa tofauti sana na kijana mmoja raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Paulen Ziarirwa mwenye umri wa miaka 28 ambaye amemuoa dada yake wa damu aitwaye, Dorica Ziarirwa mwenye umri wa miaka 26.
–
Wanandoa hawa wamezaliwa kwenye familia moja kutoka kijiji cha Bunia ambacho kilitokea mgogoro wa kikabila na kusababisha watu kuuawa na wengine kukimbia makazi yao.
Baada ya hapo akarudi kijijini kwao na walikaa hapo kwa muda mrefu hadi ikafikia wakati ambao anahitaji kujitegemea na ndipo akawaza kuishi na dada yake Dorica, mawazo hayo yakampelekea Paulen kutaka kumuoa dada yake, akaamua kumwambia dada yake kuwa anampenda na anataka kumuoa ili waanzishe familia.
–
Dorica akamwambia kaka yake Paulen kuwa inabidi wahame eneo hilo kwa sababu wanajua wao ni ndugu hivyo jamii itawachukulia tofauti, ndipo wakaamua kuhama eneo hilo na kwenda eneo linaloitwa Kashegema kisha kuanzisha familia yao.
Wanandoa hawa wakapata watoto nne na mtoto wao wa kwanza anaumri wa miaka 8 na tayari wamefikisha miaka 10 ya ndoa yao.
–
Credit : Global TV