ADVERTISEMENT
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Camillus Wambura amefanya mabadiliko madogo ndani ya jeshi hilo, ambapo amewahamisha baadhi ya makamanda wa polisi kutoka nafasi zao na kuwapangia sehemu nyingine.
–
Katika mabadiliko hayo madogo Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza, Ramadhani Ng’anzi amehamishwa na kuwa Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania.
–
Ng’anzi anachukua nafasi ya Wilbroad Mtafungwa aliyekuwa Mkuu wa kikosi hicho ambaye sasa amehamishwa na kuwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza.
ADVERTISEMENT