ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Agizo la Waziri Mkuu laibua shangwe kwa Wafanyabiashara

Dodoma, Tanzania

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Nov 28, 2022
in HABARI
0
Agizo la Waziri Mkuu laibua shangwe kwa Wafanyabiashara
0
SHARES
36
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

DKT. DUGANGE-95% YA ZABUNI ZA TARURA KAZI INAENDELEA

DKT. DUGANGE-95% YA ZABUNI ZA TARURA KAZI INAENDELEA

Jan 24, 2023

Pikipiki 916 kugawiwa kwa Watendaji wa Kata

Jan 24, 2023

DODOMA WAPONGEZWA KWA KUPIGA HATUA KWENYE ELIMU

Jan 23, 2023
Load More
May be an image of 5 people, people standing and footwear
Serikali imeziagiza Mamlaka za usafirishaji abiria Jijini Dodoma kuhakikisha daladala zote zinaanzia sokoni Machinga Complex ili kuongeza hadhi ya soko na kuinua uchumi wa Wafanyabiashara.
Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara katika soko la Machinga Complex eneo la Bahi Road Jijini Dodoma tarehe 24 Novemba, 2022 kujionea maendeleo ya soko hilo pamoja na changamoto zinazowakabili wafanyabiashara hao wadogo.
“mabasi kutoka pande zote yanayokwenda Ihumwa, UDOM, Kisasa, Msalato, yaanzie hapa, ni agizo nataka nione yanatekelezwa hayo, nikimaliza hapa Jiji na LATRA muondoke mkae, mzungumze na wafanyabiashara na wamiliki wa mabasi madogo muwaelekeze mtengeneze route (safari) ianze tuone mabasi yakiingia hapa” alisema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Aidha, Mhe. Majaliwa amemwagiza Mkurugenzi wa jiji la Dodoma kufanya vikao vya pamoja na Wafanyabiashara wadogo hao ili kufikia hatua ya makubaliano kuhusu malipo ya ushuru wa kufanya biashara katika soko hilo badala ya kuanza kutoza viwango ambavyo vitaamuliwa na upande mmoja wa Serikali.
Pia Waziri Mkuu Majaliwa amemwagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuwanyang’anya vibanda watu 28 ambao walipata vibanda viwili badala ya kimoja ili vibanda 28 wagawiwe wafanyabiashara waliokosa vibanda sokoni hapo.
Mhe. Dkt. Festo Dugange Naibu Waziri (AFYA) Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema soko hilo ni moja ya masoko 11 ambayo ni matokeo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka wafanyabiashara hao wafanyebiashara zao katika mazingira salama ili wasihangaike kwenye jua, mvua na vumbi wakiwa hali wakitembea barabarani.
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Joseph Mafuru amesema soko hilo limegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 9 (9,529,747,200) ikiwa shilingi Bilioni 6.5 ni fedha za mapato ya ndani, Bilioni 2.5 ruzuku kutoka Serikali Kuu na milioni 500 fedha za Uviko 19 kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI.
Naye Bw. Christine Msumari Kiongozi wa Wafanyabiashara ndogo ndogo katika soko la Machinga Complex amemwomba Mhe. Waziri Mkuu kuangalia namna ya kuwapatia mikopo wafanyabiashara hao bila ya kuangalia umri ambao ni kikwazo kwa baadhi ya wafanyabiashara kwani unamtambua kijana ni yule asiyezidi miaka 35.
May be an image of 6 people, people standing and food
No photo description available.
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: OFISI YA RAIS TAMISEMI
ADVERTISEMENT
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

Teknolojia Mpya ya Kupunguza Maumivu Wakati wa Hedhi
HABARI

Teknolojia Mpya ya Kupunguza Maumivu Wakati wa Hedhi

by ALFRED MTEWELE
Jan 30, 2023
WIZARA YA AFYA YATOA FURSA KWA RAIA 12 KUSIMAMIA MIRADI
HABARI

WIZARA YA AFYA YATOA FURSA KWA RAIA 12 KUSIMAMIA MIRADI

by ALFRED MTEWELE
Jan 30, 2023
NMB kupeleka washindi 8 Dubai kupitia Droo ya ‘Grand Finale’
HABARI

NMB kupeleka washindi 8 Dubai kupitia Droo ya ‘Grand Finale’

by I am Krantz
Jan 30, 2023
Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti leo Ijumaa 25.11.2022
HABARI

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Januari 30,2023

by ALFRED MTEWELE
Jan 30, 2023
WATU WENGI WALIJUA NITAVAA RANGI YA KINYOKA NYOKA – MANZOKI
HABARI

WATU WENGI WALIJUA NITAVAA RANGI YA KINYOKA NYOKA – MANZOKI

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023
SIMBA KUSHINDA UBINGWA MSIMU HUU
HABARI

SIMBA KUSHINDA UBINGWA MSIMU HUU

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
November 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
282930  
« Oct   Dec »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In