Kocha mkuu wa Mabingwa wa Tanzania, Yanga SC, Nasredeen Mohamed Nabi amelalamikia ratiba ya Ligi kuu ambayo amesema haitoi nafasi kwa wachezaji wake kupata muda wa mapumziko.
–
Yanga imecheza michezo ya ligi kuu na mechi za mtoano za Kombe la Shirikisho barani Afrika matawalia na wamerejea jana, na kesho Jumapili wanapaswa kucheza na Kagera Sugar.
–
Akizungumza za waandishi wa habari jijini Mwanza kocha Nabi amesema tangu wacheze siku ya Jumatano na Club Africain hawajapata muda wa kufanya mazoezi na kesho wanapaswa kucheza dhidi ya Kagera.
–
Licha ya ugumu huo wa ratiba, Nabi amewataka wachezaji wake kupambana na kushinda mchezo huo.
–
Kwa upande wake kocha mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Mexime amesema wapenzi wa soka watarajie burudani safi kutoka kwa vijana wake katika mchezo huo.
–
Credit : TBC