Kampuni ya Fenway Sports Group (FSG) ambayo ni wamiliki wa klabu ya Liverpool, wameiweka klabu hiyo ya Ligi Kuu England sokoni na wanakaribisha ofa kwa wanaohitaji kuinunua.
–
FSG inaipiga mnada klabu hiyo baada ya kudumu nayo kwa takribani miaka 12 tangu ilipoinunua kutoka kwa George Gillette na Tom Hicks mwaka 2010.
–
Mabingwa hao mara 6 wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya, wameanza msimu huu kwa kusuasua kwenye Ligi ya EPL licha ya kutinga hatua ya 16 ya UCL.
ADVERTISEMENT