
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Halmashauri nchini kutumia fedha za makusanyo ya ndani katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo badala ya kusubiri fedha kutoka Serikali Kuu pekee.
Amesema hayo jana (Jumapili, Novemba 27, 2022) wakati alipokagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa sita katika shule ya Sekondari ya Mwandege iliyopo Wilaya ya Mkuranga, Pwani.
Mheshimiwa Majaliwa amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mwantumu Mgonja kutenga kiasi cha shilingi milioni 120 kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo la utawala katika shule hiyo ifikapo Januari 2023.
Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba hivyo vya Madarasa, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga vizuri kuwahudumia watanzania ili kusaidia kuchochea shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
“Huu ni wakati wa kufanya kazi, nimeridhika na viwango vya ujenzi wa vyumba madarsa katika shule hii, endeleeni kusimamia viwango kwenye miradi mingine, twende na matakwa ya Rais wetu na kumsadia kutimiza maono yake ya kuwahudumia watanzania”
Waziri Mkuu amesema kuwa mipango ya Rais Samia ni kuhakikisha kwamba Serikali inawafikia watanzania popote walipo hadi vitongojini kwa kupeleka huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo afya, maji, shule, umeme pamoja na mawasiliano.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wakulima wote nchini kutumia mvua hizi za mwanzo kuanza kujishughilisha na shughuli za kulima. “Mvua za kwanza ndio mvua za kupandia, twende tukaanze kazi ya kilimo, tupande mazao yenye uwezo wa kuota kwa muda mfupi ili yaweze kuiva na kutusaidia kupata chakula”
Pia Mheshimiwa Majaliwa amewataka watendaji wa Serikali kuzungumza na wakulima kutumia vizuri chakula kilichopo ili kiweze kuwasaidia kufika msimu ujao wa mavuno.
GRANTING: USE INTERNAL REVENUE TO IMPLEMENT PROJECTS\nPrime Minister Kassim Majaliwa has asked the councils in the country to use the funds from the local collection in implementing various development projects instead of waiting for funds from the central government only.He has said this today (Sunday, November 27, 2022) when he inspected the progress of the construction of six classrooms at Mwandege Secondary School in Mkuranga District, Pwani.Honorable Majaliwa has asked the Director of the District Council of Mkuranga Mwantumu Mgonja to set aside an amount of 120 million shillings from the internal revenue for the commencement of the construction of the administrative building in the school by January 2023.Speaking after inspecting the progress of the construction of those classrooms, the Prime Minister said that the sixth phase government led by President Samia Suluhu Hassan is well organized to serve Tanzanians in order to help boost egg farming activities. versions in their areas.\n“This is the time to work, I am satisfied with the construction standards of classrooms in this school, continue to manage the standards in other projects, let us go with the wishes of our president and help him achieve his vision of serving Tanzanians”The Prime Minister has said that President Samia’s plans are to ensure that the government reaches Tanzanians wherever they are including the villages by taking various social services including health, water, schools, electricity and communication.In addition, Honorable Majaliwa has called on all farmers in the country to use these early rains to start engaging in farming activities. “The first rains are the rains for planting, let’s go and start farming, plant crops that can grow for a short time so that it can ripen and help us get food”Honorable Majaliwa has also asked government officials to talk to farmers to utilize the existing food properly so that it can help them reach the next harvest season.