Timu ya Taifa ya Tunisia imepata mapokezi makubwa ilipowasili katika mji mkuu wa Qatar, Doha tayari kwa michuano ya Kombe la FIFA la Dunia inayotarajiwa kurindima kuanzia Jumapili wiki hii.
–
Tunisia ambayo imepangwa kundi D pamoja na mabingwa watetezi Ufaransa, Australia na Denmark imewasili usiku wa kuamkia leo nchini humo.
–
Watunisia wengi wanaoishi Mashariki ya Kati pamoja na mashabiki waliosafiri, wamejitokeza kuilaki timu yao ya Taifa huku wakiwa na matumani ya kufanya vema.
–
Tunisia ni miongoni mwa Mataifa matano ya Afrika yanayowakilisha Bara hilo kwenye michuano ya Kombe la FIFA la Dunia mwaka huu.
–
Nchi nyingine ni Ghana, Morocco, Cameroon na Senegal.
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT