ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, March 28, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

WANANCHI KUWEZESHWA KUPATA HUDUMA BORA

Dodoma, Tanzania

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Nov 17, 2022
in HABARI
0
WANANCHI KUWEZESHWA KUPATA HUDUMA BORA
0
SHARES
29
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

SERIKALI YATANGAZA KUZUKA KWA UGONJWA USIOJULIKANA KAGERA

SERIKALI YATANGAZA KUZUKA KWA UGONJWA USIOJULIKANA KAGERA

Mar 17, 2023

YASTAAJABISHA: VIJANA WANAHITAJI UZA FIGO ZAO

Mar 13, 2023

MUSWADA WA BIMA YA AFYA KWA WOTE KIKWAZO TENA

Feb 9, 2023
Load More
May be an image of 4 people and people sitting
Watumishi wa Wizara ya Afya wanao wajibu wa kuwezesha jukumu kuu la kuhakikisha na kuwezesha wananchi wanapata huduma bora za afya kote nchini kwa kuhakikisha kila mmoja katika nafasi yake anafanya jukumu lake kwa ufanisi.
Hayo yamesemwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Bw. Edward Mbanga wakati wa kufungua mafunzo ya huduma kwa mteja (Customer Care) kwa watumishi wa Wizara ya Afya Makao Makuu yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma.
Bw. Mbanga amesema kuwa wananchi wote wanaofika kwenye ofisi za wizara wanatakiwa kupata huduma zinazostahili na kwa wakati bila kukwamisha mfumo wa ufanyaji kazi wa kuwahudumia wananchi.
“Yapo mambo madogo madogo ambayo yanatufanya tuonekane hatuna huduma nzuri kwa wateja, tunapaswa kuwahudumia wananchi wanaofika kwenye ofisi zetu kwani tumeajiriwa kwa ajili ya wateja hao.” Amesema Bw. Mbanga
Aidha, amewataka watumishi hao kufanya kazi bila kinyongo ama kuwakasirikia wananchi wanaofika kwenye dawati lao kanakwamba wapo kwenye biashara zao binafsi na kuonesha wapo hapo kuwahudumia wao wateja wanaokuja.
Ameongeza kuwa itakapofika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, idadi ya watu wanaoenda kutafuta huduma za afya zitaongezeka kwa sababu kutakuwa na uhakika wa matibabu hivyo inahitaji mkakati mkubwa wa kuboresha huduma kwa mteja katika utoaji wa huduma za afya kote nchini.
“Jiulize wakati ulipoaga unayemuacha nyumbani asubuhi kwamba unaenda kazini hivyo tuwaheshimu wanaokuja katika maeneo tunayofanyia kazi ili tudhihirishe kweli tupo kazini”. Alisisitiza Bw. Mbanga
Pia, Bw. Mbanga aliwataka watumishi hao kutekeleza kwa vitendo yale yote watakayoyapata kupitia mafunzo hayo na hivyo kuwa na dhamira ya kuboresha namna wanavyowahudumia wateja wao.
Naye, Mkurugenzi wa Utawala na Rasiliamali Watu, Wizara ya Afya Bi. Deodhata Makani amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa watumishi hao na kuwataka kuzingatia utoaji wa huduma bora kwa wateja wanaofika wizarani na kuongeza kuwa mafunzo hayo yameanza kwa watumishi wa makao mkauu na yatashuka hadi kwa watumishi wengine wa wizara hiyo.
#MtuNiAfya
#JaliAfyaYako
May be an image of 4 people, people sitting and headscarf
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: Wizara ya Afya
ADVERTISEMENT
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION  KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA
HABARI

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

by Ally Hamis Zingizi
Mar 27, 2023
NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
HABARI

NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

by I am Krantz
Mar 27, 2023
Naibu Waziri   aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya  michezo
HABARI

Naibu Waziri aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya michezo

by I am Krantz
Mar 27, 2023
MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA
HABARI

MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14
HABARI

BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL
HABARI

MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
November 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
282930  
« Oct   Dec »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In