
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), limetangaza matokeo ya darasa la saba ya mwaka huu, ambapo watahiniwa zaidi ya milioni 1.07 kati ya zaidi ya milioni 1.34 wamefaulu kwa kupata madaraja A na B na C.
Kati ya hao wasichana ni 558,825 na wavulana ni 514,577.
Akitangaza matokeo hayo mkoani Dar es Salaam Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Almasi amesema katika matokeo ya mwaka 2021 watahiniwa walikuwa 907,802 sawa na asilimia 81.97.
Amesema kitakwimu kuna kupungua kwa ufaulu kwa asilimia 2.35 ingawa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa watahiniwa 165, 600 sawa na asilimia 18.24 ikilinganishwa na mwaka 2021.
Mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi ulifanyika Oktoba 5 na 6 mwaka huu.
The Examination Council of Tanzania (NECTA) has announced the results of class seven this year, where more than 1.07 million out of 1.34 million candidates have passed by getting grades A, B and C. Among those, the number of girls is 558,825 and the number of boys is 514,577Announcing the results in Dar es Salaam province, the acting secretary of NECTA, Athumani Almasi has said that in the results of 2021 the candidates were 907,802 equivalent to 81.97 percent.He said that there is a decrease in success rate of 2.35 per cent although the number of successful candidates has increased to 165, 600 applicants equal to 18.24 per cent compared to 2021.The final exam of primary education was held on October 5 and 6 this year.
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT