Paris St-Germain wako tayari kumfanya mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford kuwa mmoja wa wachezaji wanaolipwa pesa nyingi zaidi katika kandanda huku wakiweka kifurushi cha kujaribu kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye mkataba wake na Manchester United unamalizika msimu wa joto. (Mirror)
Meneja wa Manchester United Erik ten Hag anasema klabu hiyo itatumia chaguo la kuongeza mkataba wa Rashford na beki wa kulia wa Ureno Diogo Dalot, 23, hadi 2024 huku wakijadili kuongezwa kwa mkataba wa wawili hao. (Metro)
ADVERTISEMENT