ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

SERIKALI KUSAIDIA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU

Pwani, Tanzania

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Dec 15, 2022
in HABARI
0
SERIKALI KUSAIDIA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU
0
SHARES
24
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

SERIKALI YAJA  NA MBINU MBADALA  KUPAMBANA NA UKATILI

SERIKALI YAJA NA MBINU MBADALA KUPAMBANA NA UKATILI

Jan 26, 2023

SERIKALI YAFUTA MASHIRIKA 4898 YASIYO YA KISERIKALI

Jan 26, 2023

KATEKISTA ADAIWA KUBAKA MWANAFUNZI

Jan 24, 2023
Load More
Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wanaosaidia watoto waishio katika mazingira magumu kwani wanasaidia ajenda ya kupunguza wimbi la watoto hao na madhara yake.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameyasema hayo akizungumza katika mahafali ya kwanza ya shule ya sekondari ya Shirika la Masista wa Maria, iliyopo Kisarawe, mkoani Pwani, Desemba 14, 2022.
Waziri Dkt. Gwajima amesema watoto wanaopitia mazingira magumu wanakumbana na hatari nyingi ikiwemo vitendo vya ukatili vinavyoathiri maisha yao na taifa kwa ujumla.
“Nimejiuliza hawa watoto wa kike wote 626 wangekuwa wapi muda huu bila shule hii, wengine wangepata ndoa na mimba za utotoni na mambo mengine ya changamoto nyingi, hivyo kuna haja ya kuunga mkono juhudi za wadau hawa ili watoto wengi zaidi wanaopitia maisha magumu wanufaike” amesema Waziri Dkt. Gwajima.
Waziri Dkt. Gwajima amesema Serikali ina mifumo ya kuwasaidia familia zilizo na maisha magumu kupitia mfuko wa TASAF lengo ambalo hata shule hii inatekeleza hivyo vema kuimarisha uratibu ili kuongeza nguvu ya kuwasaidia ambao hawajafikiwa.
Ameipongeza shule hiyo yenye mtaala wa kipekee kwani ina mtaala wa kawaida pamoja n ule wa ufundi ambao unawasaidia watoto hasa wa kike kwa kuwapa elimu ya Sekondari pamoja na ufundi kwa wakati mmoja ili wanapotoka shule wawe na ujuzi wa kuweza kujiajiri na kuajiri wengine.
Kwa upande wake Meneja wa shule hiyo yenye wanafunzi 626 Johanitha Joramu amesema, Mahafali hayo ya kwanza yana Wahitimu 142 ambao wana ujuzi mbalimbali kama kushona, kupika na ufundi umeme.
Johanitha ameongeza kwamba, mpango wa shirika ni kuongeza shule kama hiyo kwa ajili ya watoto wa kiume, jijini Dodoma.
Naye mmoja wa wahitimu wa shule hiyo Dominista Kaitani ameshukuru kwa kupata nafasi hiyo ya kupata elimu na ujuzi kwani wengi wao walikuwa hawajui hatima ya maisha yao kutokana na ugumu wa maisha.
Mahafali hayo pia yamehudhurwa na Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo aliyeongoza ibada ya misa takatifu kabla na kushiriki kugawa vyeti vya taaluma kwa wahitimu.
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII
ADVERTISEMENT
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

NMB kupeleka washindi 8 Dubai kupitia Droo ya ‘Grand Finale’
HABARI

NMB kupeleka washindi 8 Dubai kupitia Droo ya ‘Grand Finale’

by I am Krantz
Jan 30, 2023
Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti leo Ijumaa 25.11.2022
HABARI

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Januari 30,2023

by ALFRED MTEWELE
Jan 30, 2023
WATU WENGI WALIJUA NITAVAA RANGI YA KINYOKA NYOKA – MANZOKI
HABARI

WATU WENGI WALIJUA NITAVAA RANGI YA KINYOKA NYOKA – MANZOKI

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023
SIMBA KUSHINDA UBINGWA MSIMU HUU
HABARI

SIMBA KUSHINDA UBINGWA MSIMU HUU

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023
WANAFUNZI WALIOMDHALILISHA MTANDAONI  MWANAFUNZI WA CHUO CHA CDTI WAKAMATWA
HABARI

WANAFUNZI WALIOMDHALILISHA MTANDAONI MWANAFUNZI WA CHUO CHA CDTI WAKAMATWA

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023
MTOTO WA SHILOLE APATA DIVISION 1 KIDATO CHA NNE
HABARI

MTOTO WA SHILOLE APATA DIVISION 1 KIDATO CHA NNE

by Shabani Rapwi
Jan 29, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
December 2022
M T W T F S S
 1234
567891011
12131415161718
19202122232425
262728293031  
« Nov   Jan »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In