ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Monday, February 6, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

KAIRUKI AWACHARUKIA VIONGOZI, ZAIDI YA WANAFUNZI 27,000 KUTORIPOTI

Tanga

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Jan 17, 2023
in HABARI
0
KAIRUKI AWACHARUKIA VIONGOZI, ZAIDI YA WANAFUNZI 27,000 KUTORIPOTI
0
SHARES
20
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

Dkt. Jafo: “Huenda zaidi ya Sh. Trilioni 1 Zikapatikana kwa Mwaka Kutokana na Biashara ya Kaboni”

Dkt. Jafo: “Huenda zaidi ya Sh. Trilioni 1 Zikapatikana kwa Mwaka Kutokana na Biashara ya Kaboni”

Feb 3, 2023

Bilioni 213 za Miradi ya DMDP Zaistawisha Temeke

Feb 2, 2023

DKT. DUGANGE-95% YA ZABUNI ZA TARURA KAZI INAENDELEA

Jan 24, 2023
Load More
May be an image of 3 people, people standing and indoor
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Angellah Kairuki amekerwa na hali ya asilimia 55.2 ya wanafunzi waliotakiwa kujiunga na kidato cha kwanza mkoani Tanga kutoripoti shule.
Mhe. Kairuki ametoa kauli hiyo mkoani Tanga Tar 16.01.2023 wakati akizungumza na Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na viongozi wa Elimu ngazi ya Halmashauri kwenye kikao kazi cha Uboreshaji wa Usimamizi wa Elimumsingi na Sekondari katika shule ya sekondari Tanga ufundi.
Amesema takwimu za wanafunzi walioripoti kidato cha kwanza si ya kuridhisha katika mkoa huo.
“Ukiangalia kwenye elimu ya awali mpaka sasa uandikishwaji ni asilimia 82 , lakini nilitamani nisikie kwa upande wa wanafunzi wenye mahitaji maalum ni asilimia ngapi ili nao tusiwaache nyuma.”
“Kwa upande wa uwandikishwaji wanafunzi darasa la kwanza mmefikia asilimia 87.7 lakini changamoto inakuja kwenye kuripoti wanafunzi wa kidato cha kwanza.”
Amesema mpaka Januari 13, mwaka huu zaidi ya wanafunzi 27,867 ambao ni sawa na asilimia 55,2 hawajaripoti shule huku walioripoti kwa Wilaya ya Kilindi ni asilimia 11 pekee.
Mhe. Kairuki amesema mpaka sasa ni asilimia 44.8 pekee ya wanafunzi ndio wameripoti shule katika mkoa huo na kusisitiza kuwa ni lazima kila kiongozi kuhakikisha takwimu hizo zinabadilika ndani ya muda mfupi.
Amesema kati ya wanafunzi 27,867 ambao hawajaripoti shule, asilimia kubwa imechangiwa na Wilaya ya Kilindi ambayo ni asilimia 11 pekee ndio walioripoti huku Korogwe Mji ikiwa ni asilimia 22.78, Korogwe TC asilimia 30.21, Handeni TC asilimia 42.55, Handen DC asilimia 45.86, Bumbuli asilimia 53.26, Mkinga asilimia 27.98 Muhenza asilimia 50 Pangani 52 na Tanga jiji 76.23
“ Je hii ni sawa jamani? Hivyo kila mmoja kwa kadri inavyowezekana takwimu hizi zibadilike ndani ya muda mfupi sana. Haiwezekani tupo siku 16 ya mwezi wa kwanza na watoto zaidi ya 27,867 hawajaingia shule. “
“Kila mmoja arudi, ajitafakari kwa vitendo tufanye tathimini sahihi ya kufuatilia mtoto mmoja baada ya mwingine na bahati nzuri sana wengi wa wanafunzi wanatoka mkoa huu huu na wanatoka kwenye meneo yetu ambako tuna waratibu wa Elimu kata, Maafisa Elimu halmashauri, rudini katika orodha angalieni nani yuko wapi na kwa nini hajafika shuleni.”
Amesema takwimu zinaonesha kuwa Wilaya ya Lushoto ni ya mwisho katika uandikishaji wa elimu ya awali huku Pangani ikiwa na asilimia 48 na Korogwe DC ina asilimia 67 na kusisitiza haja ya kubadilika,
“Angalau tungekuwa bado mwezi mmoja kufungua shule lakini tayari watoto wamesharipoti siku saba sasa, na ukomo tuliojipangia tayari siku 16 zimepita je unatarajia ni nani ashuke afanye uhamasishaji wa uandikishaji kama sip nyie?”
Amesema kitendo cha watoto kutoandikishwa na kutoripoti kidato cha kwanza kunaondoa maana ya juhudi za Serikali za kujenga madarasa.
“ Haya madarasa tuliyoyajenga yatakuwa na maana gani, maamuzi yote tuliyofanya ya kisera yatakuwa na maana gani endapo watoto zaidi ya 27,000 ni watoto wengi sana kuwa nyumbani.”
Aidha, Mhe. Kairuki amesema kuwa masuala ya uandikishwaji wanafunzi na kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza pia amekuwa akitumia kutafsiri utendaji wa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi.
“ Mimi hizi nazitafsiri kwenye maeneo mengi, ninyi mnaweza mkaona naangalia kwenye elimu peke, inanisaidia kutafsiri kuanzia Wakuu wa Willaya na pia naangalia Wakurugenzi tulionao, shida ni nini?
“ Haya ni maeneo mengine kati ya yale 12 ya mkataba wetu wa utendaji.”
Mhe. Kairuki amesema pia kwa upande wa ufaulu wa darasa la saba na kidato cha pili, bado Tanga haifanyi vizuri na kuwataka viongozi wajitafakari kilichotokea.
“Ndugu zangu tusipobadilika tutakuwa tunamvunja moyo Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali. Rais amechukua hatua mbalimbali za kitumishi kushughulikia changamoto nyingi na kuboresha sekta ya Elimu.
May be an image of 3 people and people sitting
May be an image of 1 person and standing
May be an image of 1 person and standingMay be an image of 1 person
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: OFISI YA RAIS TAMISEMI
ADVERTISEMENT
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

DIAMOND KANILIPA MILIONI 17 VIDEO YA ZUWENA
HABARI

DIAMOND KANILIPA MILIONI 17 VIDEO YA ZUWENA

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023
VIJANA ACHENI KU-BET FANYENI KAZI – CHONGOLO
HABARI

VIJANA ACHENI KU-BET FANYENI KAZI – CHONGOLO

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023
RAIS WA ZAMANI WA PAKISTAN AFARIKI DUNIA
HABARI

RAIS WA ZAMANI WA PAKISTAN AFARIKI DUNIA

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023
IDADI YA WALIOFARIKI AJALI YA TANGA YAONGEZEKA HADI 20
HABARI

IDADI YA WALIOFARIKI AJALI YA TANGA YAONGEZEKA HADI 20

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023
MANGE KIMAMBI AMCHANA  HAJI MANARA ‘WE NI MTU MZIMA’
HABARI

MANGE KIMAMBI AMCHANA HAJI MANARA ‘WE NI MTU MZIMA’

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023
NAJUA UCHUNGU WA MTOTO SIWEZI – WOLPER
HABARI

NAJUA UCHUNGU WA MTOTO SIWEZI – WOLPER

by Shabani Rapwi
Feb 5, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
January 2023
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Dec   Feb »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In