ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Wednesday, March 22, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NMB yazindua Umebima 2023 kutoa elimu zaidi ya bima

I am Krantz by I am Krantz
Jan 31, 2023
in HABARI
0
NMB yazindua Umebima 2023 kutoa elimu zaidi ya bima
0
SHARES
15
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Kutoka Kushoto: Mkuu wa Idara ya Bima – Benki ya NMB, Martine Massawe; Kamishna wa Bima nchini, Dkt. Baghayo Saqware; Mkuu wa Mkoa wa Mbeya – Mhe. Juma Zuberi Homera na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara NMB, Filbert Mponzi wakizundua kampeni ya Umebima jijini Mbeya jana.

 

 

RelatedPosts

MECHI ZITASIMAMA EPL KUPISHA ‘IFTAR’

MECHI ZITASIMAMA EPL KUPISHA ‘IFTAR’

Mar 21, 2023

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI

Mar 21, 2023

MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA

Mar 21, 2023
Load More

 


Na Mwandishi Wetu

Katika azma yake ya kuchangia ujumuishi wa kifedha nchini kupitia huduma za bima, Benki ya NMB Jumatatu wiki hii imezindua msimu wa tatu wa kampeni ya elimu na uelewa wa masuala ya bima ya Umebima jijini Mbeya.

Kama ilivyokuwa kwa misimu ya awali, mchakato wa Umebima wa mwaka huu ni wa kitaifa na lengo lake kuu ni kuunga mkono ajenda ya taifa ya bima kwa wote.

Wakizungumza kwenye hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika Mwanjelwa-Kabwe, maafisa wa NMB walisema kampeni hiyo inashabiiana na malengo ya serikali ya kuongeza uelewa wa masuala ya bima na kuongeza matumizi ya huduma zake.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Bw. Filbert Mponzi, alisema kwa sasa uelewa wa bima nchini ni mdogo sana na kusisitiza kuwa bado kuna kazi kubwa kuhakikisha watu wengi zaidi wanakata bima kujikinga na majanga ili kuboresha kiwango cha asilimia 1.6 cha kusambaa kwa huduma hizo.

Aidha, alibainisha kuwa kimsingi kampeni ya Umebima imejikita kuyakabili mapungufu hayo kwa kuuelimisha umma kuhusu umuhimu na faida za bima hasa kwa wale ambao hawajafikiwa na huduma hiyo au kufahamu uwepo wake.

Bw Mponzi alisema tangu NMB ipate leseni ya uwakala wa bima mwaka 2020 imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia kuongeza uelewa wa bima nchini na sasa hivi watu wengi wanazidi kukata bima na kuwa na kinga ya uhakika dhidi ya majanga.

ADVERTISEMENT

Aliipongeza serikali kwa kuona mbali na kurasimisha utaratibu bunifu wa benki wakala ambao alisema umekuwa na mchango mkubwa katika kufikia malengo ya taifa ya huduma za bima kwa wote.

“Sisi kama benki wakala, ni jukumu letu kusaidia ajenda hii ya serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi ya Bima (TIRA) nchini kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanakuwa na uelewa sahihi wa bima na matumizi ya huduma zake,” Bw Mponzi alibainisha.

Kwa mara ya kwanza, kampeni ya Umebima imezinduliwa nje ya Dar es Salaam na Bw Mponzi amesema hilo limefanyika kimkakati kwani kuzinduliwa Mbeya ni sehemu ya kuhakikisha elimu ya bima inasambazwa kote nchini.
Akitolea mfano wa wahanga wa majanga ya moto ya masoko ya Mwanjelwa na Karikaoo, Bw Mponzi alisema mchakato wa Umebima umekuwa na tija kwani watu wengi wanaendelea kunufaika na kuwa na bima za maisha na mali.
“Baada ya kuungua kwa soko la Kariakoo la Dar es Salaam ndani ya wiki moja tuliwasaidia wafanyabiashara waliopoteza mali zao kulipwa fidia ya zaidi ya TZS milioni 400 na mmoja wa wadau wetu wa bima,” alifafanua.

ADVERTISEMENT

 

 


Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Bima, Bw Martine Massawe, alisema NMB ni benki wakala wa makampuni 10 ya bima kama sheria inavyoelekeza.
Kwenye hotuba yake kuzindua kampeni ya Umebima 2023, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw Juma Homera, aliipongeza NMB kwa kuongoza harakati za ukataji bima kupitia uhamasishaji mkubwa wa umma na mtandao wake mpana wa matawi 228 yaliyotapakaa nchi nzima.

“Niwapongeze sana kwa kushirikiana vyema na serikali ya mkoa wa Mbeya na ya Taifa kwa ujumla. Niwahakikishie hili la kampeni la Umebima lina baraka zetu zote kwa hiyo tuendelee kushirikiana katika ujenzi wa taifa,” Bw Homera alisema.
Uzinduzi huo uliudhuriwa pia na Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware, aliyesema kuwa kampeni ya Umebima ina maana kubwa katika maendeleo ya soko la bima nchini na uelewa wa huduma zinazopatikana ndani yake.
Kupitia kampeni hiyo, Dkt Saqware alifafanua kuwa Benki ya NMB inachangia kikamilifu kutimiza lengo la Mamlaka ya Usimamizi ya Bima la kuongeza uelewa wa huduma za bima kutoka asilimia 37 sasa hivi hadi kufikia asilimia 80 ifikapo mwaka 2030 kama Serikali inavyoelekeza.
MWISHO…

 

 

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI
HABARI

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA
HABARI

MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI WATOA MWILI WA MAREHEMU NA KUONDOKA NA SEHEMU ZA SIRI
HABARI

WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI WATOA MWILI WA MAREHEMU NA KUONDOKA NA SEHEMU ZA SIRI

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
BIKIRA JANE APATA MTOTO
HABARI

BIKIRA JANE APATA MTOTO

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
ASKARI ANAYETUHUMIWA KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE ASOMEWA MASHTAKA
HABARI

ASKARI ANAYETUHUMIWA KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE ASOMEWA MASHTAKA

by ALFRED MTEWELE
Mar 21, 2023
SEVILLA YAMFUTA KAZI KOCHA JORGE SAMPOLI NA KUMTEUA KOCHA HUYO
HABARI

SEVILLA YAMFUTA KAZI KOCHA JORGE SAMPOLI NA KUMTEUA KOCHA HUYO

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
January 2023
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Dec   Feb »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In