ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, April 2, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

WAZIRI MKUU: BUNGE BONANZA LIMEFANA

Dodoma

ALFRED MTEWELE by ALFRED MTEWELE
Jan 30, 2023
in HABARI
0
WAZIRI MKUU: BUNGE BONANZA LIMEFANA
0
SHARES
28
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

RelatedPosts

DK. TULIA ATAKA DEGREE ZISITOLEWE KAM PIPI

DK. TULIA ATAKA DEGREE ZISITOLEWE KAM PIPI

Feb 9, 2023

DKT. TULIA ACHAGULIWA UMOJA WA MABUNGE DUNIANI (IPU)

Oct 11, 2022

Naibu Waziri Maryprisca “Bei ya Unit ya Maji Haiwezi Kufanana kila Eneo”

Sep 20, 2022
Load More
May be an image of 5 people and indoorWaziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa amempongeza Spika wa Bunge Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson kwa kubuni na kulitekeleza Bonanza la kimichezo la Bunge ambalo limeanza kufanyika leo tarehe 28 Janauari, 2023 Jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa Bonanza hilo, Waziri Mkuu ambaye ndiye alikuwa Mgeni rasmi amesema kuwa bonanza hilo limefana sana na kama kuna mapungufu ni kidogo ambayo hata hivyo yatafanyiwa kazi ili bonanza lijalo liwe bora zaidi.
“Nakupongeza sana Mheshimiwa Spika kwa kubuni wazo la kuwa na bonanza na kulitekeleza. Limefana sana na kwa kuwa ndio linaanza naamini Bonanza lijalo litakuwa bora zaidi,” alisema Waziri Mkuu.
Aidha Waziri Mkuu amewaasa Waheshimiwa Wabunge na Watumishi wa Ofisi ya Bunge kutumia bonanza kama sehemu ya kufanyia mazoezi kwa ajili ya kuimarisha afya ya miili yao.
“Tunatumia muda mwingi sana kukaa wakati tunatekeleza majukumu yetu, hivyo mazoezi ya Bonanza hili yatatuweka timamu kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yetu,” alisema.
Waziri Mkuu aliongeza pia kuwa mbali na mazoezi bonanza hilo lina faida nyingine zikiwemo kujenga urafiki na kudumisha udugu miongoni mwa washiriki.
“Faida nyingine ya bonanza hili ni kukuza vipaji vya kucheza michezo mingi kwa kuwa bonanza hili linahusisha michezo mingi ambayo inatoa fursa kwa kila mmoja kushiriki,” alisema.
Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu aliwashukuru pia wadau mbalimbali ambao walifanikisha kufanyika kwa tamasha hilo wakiwemo Benki ya NMB ambao ndio walikuwa wadhamini wakuu wa bonanza la siku ya leo.
Awali akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa bonanza hilo, Spika wa Bunge Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson aliwashukuru na kuwapongeza wote walioshiriki katika tamasha hilo.
Aidha alisema bonanza hilo limeanza vizuri na kwamba changamoto ndogo ndogo zilijitokeza zitafanyiwa kazi kwa ajili ya kufanikisha mabonanza bora zaidi.
“Bonanza hili limeonesha ya kwamba tuna uwezo wa kufanya mazoezi na pia kuwahamasisha wanananchi kufanya hivyo,” alisema.
Mbali na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Watumishi wa Bunge, bonanza la leo pia lilihusisha wawakilishi kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Bonanza la Bunge la kimichezo la leo lilihusisha michezo takribani 19 ambapo kwa kiasi kikubwa Waheshimiwa Wabunge waliibuka washindi katika michezo hiyo na hivyo kuchukua vikombe vingi pamoja na Kombe la ushindi ambalo Mwenyekiti wa Bunge Bonanza Mheshimiwa Festo Sanga alikabidhiwa na Waziri Mkuu.
Bonanza hilo limepangwa kufanyika mara nne kwa mwaka ambapo bonanza lijalo linatarajiwa kufanyika tarehe 24 Juni, 2023. Kauli Mbiu ya Bonanza la leo ilikuwa: Shiriki Michezo Tujenge Taifa Lenye Afya.
May be an image of 6 people, people standing and outdoors
May be an image of 8 people, people standing and grass
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

Tags: BUNGE LA TANZANIA
ALFRED MTEWELE

ALFRED MTEWELE

Related Posts

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO
HABARI

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
CAMERA ILIYOPOTEA MIAKA 13 YAPATIKANA KWENYE MATOPE PICHA BADO ZIPO VIZURI
HABARI

CAMERA ILIYOPOTEA MIAKA 13 YAPATIKANA KWENYE MATOPE PICHA BADO ZIPO VIZURI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
AFUKUA MAITI YA MAMA YAKE NA KUKAA NAYO NDANI
HABARI

AFUKUA MAITI YA MAMA YAKE NA KUKAA NAYO NDANI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
MUUGUZI AFARIKI AKIJIFANYIA HUDUMA MWENYEWE
HABARI

MUUGUZI AFARIKI AKIJIFANYIA HUDUMA MWENYEWE

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
CHINA NA BRAZIL ZAIKATAA DOLA YA MAREKANI
HABARI

CHINA NA BRAZIL ZAIKATAA DOLA YA MAREKANI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
YANGA TUNAHITAJI KUIFUNGA MAZEMBE TUONGOZE KUNDI
HABARI

YANGA TUNAHITAJI KUIFUNGA MAZEMBE TUONGOZE KUNDI

by Shabani Rapwi
Apr 1, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
January 2023
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Dec   Feb »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In