Mshambuliaji wa Manchester City, Erling Haaland baada ya jana kufunga mabao 5 kwenye ushindi wa mabao 7-0 walioupata Man City dhidi ya RB Leipzing kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya UEFA, amefanikiwa kufikisha rekodi zifuatazo;
–
ADVERTISEMENT
Haaland amekuwa mchezaji wa tatu kufunga mabao 5, kwenye mchezo mmoja wa ligi ya mabingwa Ulaya huku akiungana na Lionel Messi aliyefanya hivyo mwaka 2012 na Luiz Adriano mwaka 2014.
–
ADVERTISEMENT
Pia amefikisha jumla ya Hat-tricks 5 msimu huu kwenye michuano yote, ikiwa ni hat-trick ya 3 zaidi ya mchezaji yoyote kwenye ligi kubwa 5 barani Ulaya msimu huu 2022-23.