ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, April 2, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

JAMII YASHAURIWA KUPIMA HOMA YA INI

Shabani Rapwi by Shabani Rapwi
Mar 16, 2023
in HABARI
0
JAMII YASHAURIWA KUPIMA HOMA YA INI
0
SHARES
20
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

RelatedPosts

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO

Apr 2, 2023

CAMERA ILIYOPOTEA MIAKA 13 YAPATIKANA KWENYE MATOPE PICHA BADO ZIPO VIZURI

Apr 2, 2023

AFUKUA MAITI YA MAMA YAKE NA KUKAA NAYO NDANI

Apr 2, 2023
Load More

 

Jamii imeshauriwa kufanya uchunguzi wa afya mapema ikiwemo Homa ya Ini ili kubaini endapo mtu ameathirika aweze kuanza tiba mapema na endapo hajaathirika aweze kupata chanjo ili kujikinga na maradhi hayo.

 

ADVERTISEMENT

 

–

 

ADVERTISEMENT

 

Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dkt. John Rwegasha kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati akifungua kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya Homa ya Ini inayofanyika Machi 15 na 16, 2023 bila malipo, zoezi linalo ratibiwa na madaktari wa Muhimbili kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
–
Dkt. Rwegasha amebainisha kuwa takwimu zinaonesha Afrika Mashariki katika kila watu 100 watu nane wanaishi na virusi vya homa ya ini ambavyo husabisha kushambuliwa kwa ini ambapo tumbo huvimba na kujaa maji.
–
“Ugonjwa huu maambukizi yake hayajioneshi moja kwa moja badala yake mtu hupata magonjwa nyemelezi ikiwemo kutapika damu au ini lake kusinyaa hivyo tumeweka kambi hii kwa lengo la kujenga uelewa kuhusu Homa ya Ini ikiwa ni kuelekea kwenye kongamano la saratani ya ini litakalofanyika Machi 17 na 18, 2023” ameongeza Dkt. Rwegasha
–
Kwa upande wake Daktari Bingwa Mbobezi Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini Dkt. Eva Uiso amesema ugonjwa wa Homa ya Ini huambukizwa na njia zake za maambukizi hazitofautiani na za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
–
Dkt.Eva ameongeza kuwa ili kuongeza uelewa kuhusu ugonjwa wa Saratani ya Ini wameamua kufanya kongamano hilo ili kujadili na kuja mikakati ya kukabiliana na ugonjwa huo nchini. Wananchi waliojitokeza kupima afya zao wameishukuru Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuweka kambi hiyo ya uchunguzi na matibabu ya homa ya ini kwani imekuwa fursa kwao kujua hali zao kiafya.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dkt. John Rwegasha akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma za uchunguzi na matibabu ya Homa ya Ini. Kushoto ni Dkt. Omari Mwanga.
Moja mwananchi akiendelea na vipimo wakati wa kambi ya uchunguzi na matibabu ya Homa ya Ini inayoendelea Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Baadhi ya wananchi wakisubiri huduma katika kambi ya uchunguzi na matibabu ya Homa ya Ini inayoendelea Muhimbili.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dkt. John Rwegasha akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Related

Shabani Rapwi

Shabani Rapwi

Related Posts

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO
HABARI

EX MSUMBUFU KUFUNGWA JELA MIAKA MITANO

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
CAMERA ILIYOPOTEA MIAKA 13 YAPATIKANA KWENYE MATOPE PICHA BADO ZIPO VIZURI
HABARI

CAMERA ILIYOPOTEA MIAKA 13 YAPATIKANA KWENYE MATOPE PICHA BADO ZIPO VIZURI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
AFUKUA MAITI YA MAMA YAKE NA KUKAA NAYO NDANI
HABARI

AFUKUA MAITI YA MAMA YAKE NA KUKAA NAYO NDANI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
MUUGUZI AFARIKI AKIJIFANYIA HUDUMA MWENYEWE
HABARI

MUUGUZI AFARIKI AKIJIFANYIA HUDUMA MWENYEWE

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
CHINA NA BRAZIL ZAIKATAA DOLA YA MAREKANI
HABARI

CHINA NA BRAZIL ZAIKATAA DOLA YA MAREKANI

by Shabani Rapwi
Apr 2, 2023
YANGA TUNAHITAJI KUIFUNGA MAZEMBE TUONGOZE KUNDI
HABARI

YANGA TUNAHITAJI KUIFUNGA MAZEMBE TUONGOZE KUNDI

by Shabani Rapwi
Apr 1, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
March 2023
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In