ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

ACHANGIWA MIL. 245 NA MASHABIKI WA KLABU YAKE YA ZAMANI BAADA YA KUTUMA SMS KATIKA TV

Shabani Rapwi by Shabani Rapwi
Apr 24, 2023
in HABARI
0
ACHANGIWA MIL. 245 NA MASHABIKI WA KLABU YAKE YA ZAMANI BAADA YA KUTUMA SMS KATIKA TV
0
SHARES
2k
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Golikipa wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika Kusini na klabu ya Kaizer Chiefs, Emile Baron amepokea msaada wa kiasi cha pesa zaidi ya Milion 245 kutoka kwa mashabiki wa klabu yake ya zamani ya Lillestrøm ya Norway baada ya kufahamishwa kuhusu hali ya kusikitisha ya mchezaji huyo aliyestaafu.

 

RelatedPosts

No Content Available
Load More

Baron alicheza soka la kulipwa mara ya mwisho katika mechi kati ya Bidvest Wits dhidi ya Orlando Pirates alipovunjika mguu tarehe 27 Aprili 2013. Tangu wakati huo ameangukia katika umaskini na kuhangaika kutafuta riziki kwa mke wake na wanawe wawili.

 

Baron alikiri kwamba mambo yalikuwa mabaya sana alijaribu kujiua mara nne, mara ya mwisho mnamo Novemba mwaka jana 2022 kutokana na maisha kuwa magumu, pia alifukuzwa kutoka kwa nyumba ndogo ya chumba kimoja na kulala barabarani

 

 

“Mambo ni mabaya zaidi sasa. Mimi na mke wangu tumekuwa tukilala barabarani, watoto wanaendelea vizuri hadi sasa,” Baron aliandika kupitia SMS na kutuma TV 2 ya Norway

 

Waliposikia habari za kusikitisha kuhusu hali ya Baron, mashabiki wa Lillestrøm, klabu ambayo Baron aliichezea kati ya 1999 na 2005, walitoa wito wa kuwepo kwa mchango mkubwa nchini Norway, huku michango ikitoka kwa karibu watu 5,000.

 

“Kuna watu wengi wamesikitishwa sana kusikia hali ya Emile anavyoishi sasa. Watu wengi, wengi wanaotaka kuchangia,” Morten Stokstad, meneja w habari na mawasiliano wa Lillestrøm aliiambia TV 2 baada ya klabu hiyo kuungana na kundi rasmi la mashabiki wanajiita “Kanari-Fansen”.

 

Baron, alionekana kushangakwa kiasi kikubwa cha uungwaji mkono aliopokea kiasi hiko cha pesa kwa kusema “Sina la kusema. Sijui jinsi ya kutoa shukrani zangu, ni kubwa sana. Asante sana,” aliambia TV 2 kwenye SMS nyingine.

 

 

Takriban Kr1,1 Milion ( sawa na Shilling Milion 243 za Kitanzania) zilikusanywa kutoka kwa mashabiki na watu wa Lillestrøm kote nchini Norwe, kama ilivyoripotiwa na TimesLIVE.

 

Baron alifunguka kuhusu matatizo yake ya kifedha mwaka wa 2019, akisema hakupokea pesa za bima kutoka kwa PSL baada ya jeraha lake. Pia alisema vilabu vya ndani havikujibu maombi yake ya usaidizi.

 

Mchezaji huyo ambaye sasa ana umri wa miaka 43 alianza uchezaji wake katika klabu ya Hellenic mwaka wa 1996, kabla ya kuhamia Lillestrøm baada ya kurejea Afrika Kusini, alichezea Kaizer Chiefs kati ya 2005 na 2009. Kisha akajiunga na SuperSport United kwa misimu miwili, kabla ya miaka miwili akiwa Bidvest Wits kabla ya jeraha lake la mwisho la soka.

 

 

Alishinda ubingwa wa Ligi Kuu Afrika Kusini akiwa na SuperSport mnamo 2009/10 na kuiwakilisha Bafana Bafana mara sita, ikijumuisha mara mbili kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika la 2004.

 

 

 

NB : Hili ni somo na funzo kwa wachezaji wetu wa Tanzania kujikatia bima ya Afya ni muhimu sana katika kipindi cha uchezaji wako, pia ni muhimu sana kwa mchezaji kuondoka katika klabu vizuri kwa nidhamu ili hata pindi utakapopata matatizo wakuunge mkono kwa kutambua mchango wako. Pia ili soma kwa mashabiki kuthamini mchango wa wachezaji wao wa zamani.  Imeandikwa na Shabani Rapwi ( Nyota wa Mchezo).

Related

Tags: Bidvest WitsEmile BaronimesLIVEKaizer ChiefsLillestrømOrlando PiratesSuperSport United
Shabani Rapwi

Shabani Rapwi

Related Posts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy
BIASHARA

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

by I am Krantz
Sep 22, 2023
DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA
HABARI

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA
HABARI

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA
AFYA

MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST
HABARI

SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO
HABARI

TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

April 2023
M T W T F S S
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In