Mahakama ya wilaya ya Kilwa imemhukumu Muharami Hassan Nayonga, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumkuta na hatia ya kuruhusu kuingiliwa kinyume na maumbile na watu mbalimbali.
–
Muharami ambaye ni mlinzi wa SUMA JKT na mkazi wa Kata ya Masoko, alikamatwa Aprili 13, 2023, baada ya kumshawishi kwa kutumia simu, kijana anayefahamika kwa jina la Zalafi Selemani ili aweze kumuingilia kinyume na maumbile.
ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT
–
Baada ya kukamatwa, mtuhumiwa alichunguzwa na wataalamu wa Afya ambao walibaini kuwa kijana huyo hushiriki ngono kinyume na maumbile.