ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NMB ‘yawapiga msasa’ wanawake wa TUICO – Morogoro

I am Krantz by I am Krantz
May 2, 2023
in HABARI
0
NMB ‘yawapiga msasa’ wanawake wa TUICO – Morogoro
0
SHARES
97
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa benki ya NMB, Joanitha Mrengo(Kulia) akizungumza na Naibu Katibu Mkuu TUICO, Takim Salehe(Kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Mashirika ya Fedha TUICO, Peles Jonathan Hageze(Katikati) baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wanawake wanachama wa TUICO – Morogoro.

 

RelatedPosts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Sep 22, 2023

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

Sep 21, 2023

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

Sep 21, 2023
Load More

Wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri Tanzania (TUICO), wametakiwa kuvutiwa na mafanikio kitaifa na kimataifa ya Hati Fungani ya Jasiri ya Benki ya NMB ‘NMB Jasiri Bond,’ na kuyatumia kama chachu ya kuendelea kuwa wateja waaminifu wa benki hiyo ili kuwa sehemu ya mnyororo wa wanufaika wa huduma zenye lengo la kusaidia ustawi wao kimaisha na kukua kiuchumi.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa Benki ya NMB, Joanitha Mrengo, alipomwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna, katika semina ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wanawake ambao ni Wanachama wa TUICO Mkoa wa Morogoro, iliyofanyika kwa siku moja, ikihudhuriwa pia na viongozi wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na Shirika la Kazi Duniani (ILO) na kudhaminiwa na benki hiyo.

Aprili mwaka jana, NMB ilihitimisha mauzo ya Hati Fungani ya Jasiri kwa kuvuna kiasi cha Sh. Bil. 74 na kuvuka lengo la kukusanya Shilingi bilioni 25 pesa zilizotumika kutanua wigo wa utoaji huduma za mikopo kwa kampuni zinazoendeshwa na wanawake, ama kampuni zinazozalisha bidhaa zinazowagusa wanawake nchini.

Ni mafanikio yaliyoipa NMB tuzo mbalimbali, zikiwemo za Hati Fungani Bora ya Mwaka iliyotolewa na Waandaaji wa Tuzo za Kimataifa za Mitaji kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kwa kushirikiana na Jukwaa la Ufadhili wa Ujasiriamali (SME’s Finance Forum), pamoja na Tuzo ya Platinum ya Kundi la Dhamana Endelevu iliyotolewa nchini Cambodia, kote ikitambulika kama hati fungani wezeshi kwa wanawake, kiasi cha kuorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Luxemburg (LuxSE), ambalo ni moja ya masoko makubwa ya hisa duniani.

Akizungumza wakati akifungua semina hiyo, Mrengo alisema mafanikio hayo, pamoja na kutambuliwa kwa benki yake kuwa miongoni mwa taasisi kinara katika mgawanyo wa kiuchumi kwenye suala la kijinsia (EDGE Certificate), ambako NMB ni taasisi ya kwanza Afrika kutunukiwa cheti, vinapaswa kutazamwa kwa jicho la ziada na wanawake wote nchini, wanaopambania ukuaji wao kiuchumi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa TUICO, Tamim Salehe, aliishukuru NMB kwa kushirikiana na chama chake katika kuwanoa wanawake wanachama wa mkoa wa Morogoro, huku akiwataka washiriki wote kuitumia vema semina hiyo sio tu kwa kuzingatia maelekezo, bali pia kujenga mtandao wa kiushirikiano baina yao ili kusaidiana maarifa ya utatuzi wa changamoto mahali pa kazi ama biashara zao.

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy
BIASHARA

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

by I am Krantz
Sep 22, 2023
DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA
HABARI

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA
HABARI

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA
AFYA

MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST
HABARI

SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO
HABARI

TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

May 2023
M T W T F S S
1234567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In