ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

RC Dar azindua Huduma ya NMB Onja Unogewe, aiita akili kubwa

I am Krantz by I am Krantz
Jun 27, 2023
in HABARI
0
RC Dar azindua Huduma ya NMB Onja Unogewe, aiita akili kubwa
0
SHARES
78
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

RelatedPosts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

Oct 2, 2023

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

Oct 2, 2023

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

Oct 2, 2023
Load More

 

NA MWANDISHI WETU

BENKI ya NMB imezindua huduma mpya chini ya Mwamvuli wa Teleza Kidigitali iitwayo NMB Onja Unogewe, ambayo imepongezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, aliyeitaja kuwa ni zao la akili kubwa na ubunifu wa wafanyakazi wa benki hiyo, unaoenda kuihakikishia jamii njia rahisi na salama ya kupokea fedha na kufanya malipo.

Sambamba na hayo, RC Chalamila ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi uliofanyika Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam, alisema NMB Onja Unogewe ni huduma chanya iliyovuka mstari wa huduma za kibenki na kwamba Serikali inaitarajia itaenda kuwa chachu ya kukuza elimu ya uhifadhi na matumizi sahihi ya fedha kwa Watanzania.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, RC Chalamila alisema Serikali inapongeza ubunifu wa suluhishi za kifedha unaofanywa na NMB, huku akiitaja huduma hiyo kuwa ni muarobaini wa upotevu wa pesa, uporaji, wizi, matumizi yasiyo ya lazima na hatarishi nyinginezo zitokanazo na matumizi ya pesa taslimu.

“Mtaji mkubwa wa NMB tangu ilipoanzishwa (1997) hadi sasa inapokuwa kinara wa huduma za kifedha nchini, ni watumishi wabunifu, walio na akili kubwa za kufikiria suluhishi sahihi, rahisi, nafuu na salama za kifedha kama hizi. Kwa miaka yote hiyo, benki ‘imeji-transform’ yenyewe na hiyo kuwa chachu ya kupaa kwao kimafanikio.

“Kuna matarajio makubwa ya kufanya vizuri mara 20 ya ilivyo sasa katika miaka kadhaa ijayo, kwa sababu NMB inaziona changamoto zitokanazo na matumizi ya pesa taslimu kuwa ni fursa, ikaja na suluhishi hizi hizi za kidigitali kusaidia jamii kuachana na utamaduni wa matumizi yasiyo sahihi na kuongeza uhifadhi wa fedha zao,” alisema RC Chalamila.

Aliwataka watoa huduma mbalimbali za kijamii wakiwemo waendesha bodaboda, bajaji, mama lishe, wauza maduka, wafanyabiashara na wajasiriamali wa kada zote jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa ya NMB Onja Unogewe kwa kupata QR Code zao na kuzitumia kwa ustawi na ukuaji wao kiuchumi.

“Achaneni na utamaduni wa kutunza fedha kwenye vibubu majumbani ama kuweka madukani, ambako hatari za upotevu, wizi ama ajali za matukio ya kuunguliwa moto ni nyingi, kimbilieni katika suluhishi hizi matawini, chukueni QR Code zenu na mfanye malipo kupitia hizo kwa usalama wa pesa za mtu mmoja mmoja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa,” alisisitiza.

Awali, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema benki yake inajivunia sana bunifu za suluhishi za kifedha, alizozitaja kuwa ni siri ya mafanikio ya benki hiyo, ambayo mwaka jana uliuongezea thamani Mwamvuli wa Teleza Kidigitali ulioanzishwa mwaka 2019 kwa kuizindulia Huduma ya NMB Pesa Wakala – huduma maalum ya kuweka na kutoa pesa kirahisi kupitia mawakala wanaotumia simu za mkononi.

“NMB Onja Unogewe ni maboresho ya Huduma ya Lipa Mkononi ‘QR Code,’ ambayo yanaenda kumpa wigo mpana mteja wa kulipia huduma kwa njia ya kidigitali, ambako atanufaika na rejesho la asilimia 10 katika malipo yake.    Tunafanya hivyo kwa makusudi ili kuvutia zaidi watumiaji wa huduma zetu za kimtandao ili kupunguza matumizi ya pesa taslimu.

“Pamoja na suluhishi hizi zote tunazobuni, kuzindua na kutoa kwa Watanzania, bado tunao utamaduni endelevu wa kurejesha kwa jamii katika sekta za elimu, afya na mazingira.

“Tayari tumepanda miti 500,000 kupitia Kampeni Endelevu ya Upandaji Miti Milioni 1 mwaka huu wa 2022, pamoja na misaada kwenye mashule na hata Hospitali zetu, ikiwemo ya Taifa ya Muhimbili ambako tumeingia makubaliano ya kuboresha Wodi ya Uzazi na tumetumia zaidi ya Sh. Mil. 250,” alibainisha na kusema Dar wametumia zaidi ya Mil. 80 katika elimu.

Kwa niaba ya NMB, Mponzi aliahidi kwamba benki hiyo itaendelea kuwa bega kwa bega na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kutatua kero na changamoto zinazokwaza ustawi wa elimu na huduma za afya nchini, huku akiwataka watoa huduma za bodaboda, bajaji, mama lishe, wauza maduka, wafanyabiashara na wajasiriamali kufika matawini kupata QR Code zao.

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10
HABARI

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
HABARI

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM
HABARI

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI
BIASHARA

MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA
HABARI

SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA
HABARI

TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

June 2023
M T W T F S S
 1234
567891011
12131415161718
19202122232425
2627282930  
« May   Jul »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In