ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NSSF YATENGENEZA FAIDA YA ZAIDI YA TRILIONI 1.01 MWAKA 2021/22 KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA

I am Krantz by I am Krantz
Jul 14, 2023
in HABARI
0
0
SHARES
67
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NSSF YATENGENEZA FAIDA YA ZAIDI YA TRILIONI 1.01 MWAKA 2021/22 KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA

*Yasema mafanikio hayo yamechangiwa na Serikali ya awamu ya sita kuvutia wawekezaji

Na MWANDISHI WETU

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepata faida ya zaidi ya shilingi trilioni 1.01, kulingana na hesabu zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika mwaka wa 2021/22, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba amesema.

Amesema sambamba na hilo pia mapato yatokanayo na uwekezaji nayo yameongezeka na kufikia shilingi bilioni 745. “Hii haijawahi kutokea katika historia ya NSSF” amebainisha Mkurugenzi Mkuu wakati akitoa tathmini yake baada ya kupokea taarifa ya watendaji wa Mfuko walioshiriki kuhudumia wanachama na wananchi kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yaliyofikia kilele Julai 13, 2023.

Mshomba ametaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye mara tu baada ya kuingia madarakani alikuja na mpango  wa “Kuifungua Nchi” akilenga kuwaalika wawekezaji kuja kuwekeza nchini lakini pia kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko Tanzania kupitia filamu ya “The Royal Tour”.

“Kichocheo kikubwa ni Mheshimiwa Rais alivyoweza kuwavuta wawekezaji, kumekuwa na ongezeko kubwa la waajiri na waajiriwa, suala zima la uchangiaji limeongezeka, vipato vya wafanyakazi vimeongezeka na haya yote yamechangia kuongeza michango na kufanya kipato cha Mfuko kutokana na uwekezaji kuongezeka pia.” alifafanua  Mshomba

Alisema sababu nyingine ni juhudi kubwa zilizowekwa na Mfuko katika kuboresha mifumo ya TEHAMA ambayo imesaidia kuboresha utoaji wa huduma.

“Kulingana na Mpango wetu wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambao unaishia Juni 2026, thamani ya Mfuko itafikia zaidi ya trilioni 11.5, na yote haya yanatokana na msukumo wa kuongeza waajiri na waajiriwa wanaochangia katika Mfuko lakini pia kazi nzuri inayofanywa na Mfuko.” alifafanua.

Kwa sasa thamani ya Mfuko wa NSSF ni trilioni 7.1, hivyo Mkurugenzi Mkuu  amewahimiza  Watanzania hususan kutoka sekta binafsi  kujiunga kwa wingi ili kujenga maisha yao ya sasa na ya baadaye.

Aidha, Mshomba amesema NSSF imepewa jukumu la kushughulika na sekta isiyo rasmi.
“Tunakamilisha taratibu za mwisho na tunaamini tukiweza kuwa na uchangiaji katika sekta isiyo rasmi, basi NSSF itazidi kupaa zaidi na kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi hii.” alisema

Alisema idadi kubwa ya Watanzania wako katika sekta isiyo rasmi na wakiweza kujumuishwa kwenye mpango huo wa taifa litakuwa limefanikiwa kuondoa umaskini nchini.

“Kama ninavyosema siku zote hifadhi ya jamii iko kwa ajili ya kuwahudumia wananchama hasa kwa lengo la kuwaondolea umaskini pale wanapokoma kufanya kazi.” Alifafanua.

Kuhusu ushiriki wa NSSF katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, Bw. Mshomba amesema wanachama zaidi ya 2,400 wametembelea na kuhudumiwa katika banda hilo kwa siku zote za Maonesho.

“Kumekuwa na mabadilio chanya ukilinganisha na mwaka jana, Wanachama wetu wamehudumiwa kwa kupatiwa elimu, usajili wa Wanachama, umuhimu wa kuwasilisha Michango kwa wakati na kuondoa kero mwanachama anapostaafu, elimu katika masuala ya uwekezaji, Mafao yatolewayo na Mfuko ambayo yanafikia saba lakini pia masuala ya Uwekezaji.” alifafanua.

Kuhusu Uwekezaji,  Mshomba amesema wamebaini kuwa watu wengi wamevutiwa na eneo hilo.

“Kuna maeneo ambayo wanachama wetu wanaweza kufaidika moja kwa moja tunajenga nyumba na kuuza, au kupangisha kwa wateja.Hivyo aliendelea kwa kutoa rai kwa Watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali za NSSF.

RelatedPosts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

Sep 29, 2023

TSO WAZINDUA GALA DINNER

Sep 29, 2023

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

Sep 29, 2023
Load More

Mkurugenzi Mkuu wa  Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba ametembelea banda namba 13 la ushirikiano baina ya NSSF na PSSSF kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mfuko na kufurahishwa na huduma zote ambazo zilikuwa zinatolewa  katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam ‘Sabasaba’ yaliyofungwa na Mhe. Dkt. Husaein Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, tarehe 13 Julai2023, katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba akizungumza na mwanachama aliyetembelea katika banda la Mfuko, ambapo alimueleza kuwa pamoja na kuwa mwanachama wa sekta binafsi lakini bado anaweza kuchangia kwa hiari kupitia sekta isiyo rasmi kwa kuwa ina manufaa.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, akizungumza jambo na mwanachama William Matee, aliyejiunga na huduma ya NSSF Taarifa Mobile App, ambapo sasa anaweza kutazama michango yake bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Matukio katika picha

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO
HABARI

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TSO WAZINDUA GALA DINNER
HABARI

TSO WAZINDUA GALA DINNER

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
CHANJO YA MBWA NI MUHIMU
AFYA

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN
HABARI

52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA
HABARI

SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 
HABARI

TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 

by I am Krantz
Sep 29, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

July 2023
M T W T F S S
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
31  
« Jun   Aug »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In