ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NMB yadhamini CDF Trophy 2023 kwa Mil. 30/-

I am Krantz by I am Krantz
Aug 22, 2023
in HABARI
0
NMB yadhamini CDF Trophy 2023 kwa Mil. 30/-
0
SHARES
20
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi NMB – Aikansia Muro akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni 30 kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu ya Lugalo – Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo ikiwa ni udhamini wetu wa mwaka huu. Makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania (TGU) – Gilman Kasiga; Kapteni wa Klabu ya Gofu ya Lugalo – Meja Japhet Masai na Meneja Mwandamizi wa Idara ya Wateja Binafsi NMB – Priscus Kavishe.

NA MWANDISHI WETU

RelatedPosts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Sep 22, 2023

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

Sep 21, 2023

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

Sep 21, 2023
Load More

BENKI ya NMB, imetangaza udhamini wa Sh. Milioni 30 wa Mashindano ya Gofu ya Mkuu wa Majeshi Tanzania (NMB CDF Trophy 2023), yanayotumika kuadhimisha miaka 59 ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ).

Huu ni msimu wa nane mfululizo kwa NMB kudhamini CDF Trophy, mashindano ya wazi yatakayofanyika Septemba 2 na 3 kwenye Viwanja vya Gofu Lugalo, ambapo mwaka huu yatatanguliwa na Mashindano ya Majeshi (Combat Fiddle), hapo Septemba Mosi, yakishirikisha timu za Majeshi ya Tanzania na Malawi.

Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi ya mfano kwa Brigedia Jenerali Mstaafu, Michael Luwongo ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu Lugalo (TPDF Lugalo Golf Club – inayoandaa mashindano hayo), Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi wa NMB, Aikansia Muro, alisema benki yake inajisikia fahari kwa aina ya mashirikiano mema yaliyopo baina yao na JWTZ yanayowasukuma kuendelea kudhamini.

“Tunaishukuru Lugalo Golf Club na JWTZ kwa ujumla, kwa ushirikiano mwema na endelevu baina yetu, ambao umetupa heshima ya kudhamini CDF Trophy kwa miaka nane sasa. Udhamini huu endelevu unaodhihirisha kuwa kuna mahusiano mazuri baina ya NMB na JWTZ, unachagizwa pia na dhamira yetu ya kutambua umuhimu wa michezo kwa jamii.

 

“Katika kufanikisha mashindano haya mwaka huu JWTZ inapoadhimisha miaka 59 hapo Septemba Mosi, NMB tumetoa Sh. Milioni 30 kufanikisha michuano hii ya mwaka huu.

“Huu ni muendelezo wa benki yetu kudhamini michezo nchini, ambako karibuni tu tumesaini makubaliano ya kuongeza ufanisi wa usajili wa Mashabiki na Wanachama wa klabu kongwe za soka za Yanga na Simba, huku tukiwa na kumbukumbu chanya za kuzidhamini Taifa Stars, Azam FC, Singida United, timu ya Taifa ya mpira wa magongo na Mashindano ya mashule,” alibainisha Aikansia.

Kwa upande wake, Brigedia Jenerali Mstaafu, Luwongo, aliishukuru NMB kwa kuyabeba mashindano hayo kila mwaka wanapokuwa katika Maadhimisho ya Kuanzishwa kwa JWTZ Septemba 1, 1964 na kwamba pamoja na shughuli mbalimbali za kijeshi zinazofanyika, wao kama klabu ya Gofu ya Jeshi hilo, wanaadhimisha kwa mashindano ya kumuenzi Mkuu wa Majeshi (CDF).

 

“Tunawashukuru na kuwapongeza NMB kwa ushiriki wao katika mashindano haya, ambayo yatakuwa ya wazi yakishirikisha timu za Jeshi la Tanzania, Malawi na timu za kiraia, yakitangukiwa na Combat Fiddle Ijumaa ya Septemba 1.

“Malawi ambao walishiriki pia mwaka jana, watakuja na timu za Jeshi lao, lakini pia Klabu ya Gofu ya Lilongwe (Lilongwe Golf Club) ambayo ni ya kiraia, msafara wao utajumuisha takribani washiriki 20, huku tayari washiriki wa ndani wapatao 100 wakiwa wameshajisajili.

“NMB CDF Trophy ni shindano la kipekee kabisa, ambalo litakuwa na zawadi nzuri zilizoboreshwa zaidi kwa ajili ya washindi wa kategori zote za ‘Professional,’ Watoto (juniors), Divisheni za A, B na C, pamoja na wanawake na ‘seniors.’

“Tutaitumia NMB CDF Trophy kuiandaa timu ya Taifa ya Tanzania ya Gofu itakayoshiriki Mashindano ya Jumuiya ya Madola, huko San Diego, Marekani, ambako Afrika itakuwa nchi pekee kuiwakilisha Afrika,” alisema Brigedia Jenerali Mstaafu Luwongo.

Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania (TGU), Gilman Kisiga, aliipongeza NMB kwa udhamini uliotukuka unaolenga kuhamasisha maendeleo na kukuza mchezo huo nchini, huku Nahodha wa Klabu ya Gofu Lugalo, Meja Japhet Masai, akijinasibu utayari wa kikosi chao na kwamba watautumia uenyeji wao kutwaa mataji ya mashindano hayo ya wazi yatakayosimamiwa na TGU.

Mwisho

 

 

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy
BIASHARA

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

by I am Krantz
Sep 22, 2023
DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA
HABARI

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA
HABARI

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA
AFYA

MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST
HABARI

SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO
HABARI

TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

August 2023
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In