ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

POLISI YAKAMATA MAWE YA DHAHABU

By Shukran Suzo - Aug 23, 2023 In Habari

SUZO SHUKRANI by SUZO SHUKRANI
Aug 23, 2023
in HABARI
0
POLISI YAKAMATA MAWE YA DHAHABU
0
SHARES
68
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema Jeshi la Polisi Mkoani humo limekamata mawe yenye madini ya dhahabu yenye uzito wa gramu 6753.4 na thamani ya shilingi bilioni 9.2 yakitoroshwa kutoka kwenye mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu wilayani Kahama huku pia likikamata Carbon yenye mchanga wenye madini yanayodhaniwa kuwa ni dhahabu yenye uzito wa Kg 261 ambayo thamani yake bado haijajulikana katika maeneo ya Manzese Kahama.

RelatedPosts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

Oct 2, 2023

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

Oct 2, 2023

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

Oct 2, 2023
Load More

 

ACP Janeth Magomi ameyasema hayo mbele ya vyombo vya habari leo Jumatano Agosti 23,2023 kuwa mali hizo zimekamatwa kwa kipindi cha kuanzia julai 26 hadi Augusti 22 baada ya kufanya misako na doria katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Shinyanga.

“Pia tumekamata jumla ya lita 603 za mafuta aina ya Diesel katika maeneo tofauti ya mradi wa Reli ya mwendokasi SGR. Mafuta haya yamewekwa kwenye chupa ndogo, wezi wa mafuta sasa hivi wamebuni mbinu ya kutumia vichupa badala ya madumu makubwa”, amesema Kamanda Magomi.

 

Amesema , katika misako hiyo Jeshi la polisi Shinyanga pia limefanikiwa kukamata Bunduki aina ya Riffle yenye namba 2/49PF78701 ambayo ilikuwa inatumika katika shughuli za ulinzi bila kibali.

 

Vitu vingine vilivyokamatwa na jeshi la polisi ni dawa za kulevya aina ya Bangi yenye uzito wa Kg 71, seti moja ya computer, Pikipiki 03, tiles Box 14, mabomba 06 ya chuma na vipande 09, Mabati 17, Plastic 3 za rangi ya majumba, mifuko 02 ya Cement, mifuko 7 ya chokaa, pamoja na Pakti 120 za vipodozi vinavyoaminika kuwa na sumu.

 

Kamanda Magomi amesema, jumla ya watuhumiwa 31 wanashikiliwa katika vituo mbalimbali vya Polisi kuhusiana na makosa hayo na wengine wamepewa dhamana huku wakisubiri kufikishwa mahakamani.

 

#KonceptTVUpdates

Related

SUZO SHUKRANI

SUZO SHUKRANI

Related Posts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10
HABARI

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
HABARI

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM
HABARI

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI
BIASHARA

MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA
HABARI

SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA
HABARI

TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

August 2023
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In