ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

Rais Samia aipa cheti NMB cha mlipa gawio mkubwa

I am Krantz by I am Krantz
Aug 21, 2023
in HABARI
0
Rais Samia aipa cheti NMB cha mlipa gawio mkubwa
0
SHARES
81
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dkt. Edwin Mhede Cheti cha Mlipa gawio kubwa serikalini wakati wa kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma jijini Arusha. Benki hiyo ambayo serikali ina miliki asilimia 31.8, ilitoa gawio la biliioni 45.5 mwaka wa fedha 2021- 2022.

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dkt. Edwin Mhede Cheti cha Mlipa gawio kubwa serikalini wakati wa kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma jijini Arusha. Benki hiyo ambayo serikali ina miliki asilimia 31.8, ilitoa gawio la biliioni 45.5 mwaka wa fedha 2021- 2022.

**

RelatedPosts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

Oct 2, 2023

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

Oct 2, 2023

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

Oct 2, 2023
Load More

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan ametoa tuzo maalum kwa Benki ya NMB katika kutambua mchango na utendaji mzuri wa taasisi hiyo ya fedha nchini.

Akizungumza katika kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma kinachofanyika katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha, Rais Samia amesema pamoja na kuwapongeza wale waliofanya vizuri, serikali pia itafanya tathmini ya utendaji wa taasisi na mashirika mengine nchini.

“Kupitia mashirika, serikali inaweza kukusanya fedha nyingi za kutosha kujazia upungufu wa bajeti ya nchi na hivyo kuipunguzia serikali mzigo wa kwenda kukopa nje,” alisema Dkt. Samia.

“Ni muhimu sana ofisi ya msajili wa hazina ihakikishe inasimamia ipasavyo sheria na kanuni zilizopo katika kuhakikisha kuwa taasisi za umma zinajiendesha kwa tija na kuipunguzia serikali mzigo wa gharama za kuziendesha,” alisema Rais Samia.

Pamoja na kutoa pongezi kwa Benki ya NMB, Rais Samia pia amemkabidhi cheti cha mlipa gawio kubwa serikalini katika sekta ya kibenki, Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo ya fedha Ruth Zaipuna.

Benki ya NMB imetoa gawio la shilingi Billioni 45.5 serikalini katika mwaka wa fedha uliopita.

Kwa mujibu wa Msajili wa Hazina, Nehemiah Kyando Mchechu, Serikali inamiliki asilimia 31.8 ya hisa katika benki ya NMB.

“Tumetoa tuzo kwa taasisi zilizofanya vizuri ili kuleta changamoto katika kujifunza sisi sote na ili taasisi zingine ziwe na wivu wa kusonga mbele ndio tuweze kuisaidia nchi yetu,” alisema Mchechu.

Kwa mujibu wa Msajili huyo wa Hazina, serikali imewekeza zaidi ya shilingi trillioni 73 katika taasisi za umma na kwamba ni jukumu lao kuhakikisha fedha hizo zinazaa matunda makubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

“Tunatarajia kuwa siku za mbeleni pamoja na kuwa na list of fame (orodha ya sifa), ya taasisi zinazofanya vizuri, baadae pia tungeweza kuwa na list of shame (ordha ya aibu) kwa taasisi zinazofanya vibaya lakini hatutarajii kufika huko, kutokana na maboresho makubwa tunayofanya kwa taasisi hizi kwa sasa,” alisema Mchechu.

Jumla ya taasisi 248 zimeshiriki mkutano huo wa kwanza wa mwaka wa kikao Kazi cha wenyekiti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma ukiwa na washiriki Zaidi ya 600.
**Mwisho.

 

 

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10
HABARI

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
HABARI

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM
HABARI

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI
BIASHARA

MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA
HABARI

SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA
HABARI

TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

August 2023
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In