ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

TUNISIA NA LIBYA WAKUBALIANA KUTOA HIFADHI KWA WAHAMIAJI

Dar es salaam

HIJA SELEMANI by HIJA SELEMANI
Aug 14, 2023
in HABARI
0
TUNISIA NA LIBYA WAKUBALIANA KUTOA HIFADHI KWA WAHAMIAJI
0
SHARES
27
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Nchi ya Tunisia na Libya zimetangaza makubaliano ya kushirikiana na wajibu wa kutoa hifadhi kwa mamia ya wahamiaji ambao wamekwama mpakani, huku wengi wao wakiwa wamekwama kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Mashirika ya misaada yanasema makundi matatu ya takriban wahamiaji 300 kutoka nchi za Afrika chini ya jangwa la Sahara kwa ujumla walikwama huko na kuishi katika hali ya kutishia maisha yao.

RelatedPosts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Sep 22, 2023

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

Sep 21, 2023

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

Sep 21, 2023
Load More

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya Tunisia, Faker Bouzghaya anasema kuwa wakati wa kikao cha pamoja na maafisa wa Libya mjini Tunis, wamekubaliana kushirikiana na makundi hayo ya wahamiaji ambao wako mpakani. Pia anasema Tunisia itachukua jukumu la kundi la wanaume 76, wanawake 42 na watoto 4.

Faker anasema makundi hayo yalihamishwa siku ya Jumatano na kupelekwa kwenye vituo katika miji ya Tatouine na Medenine na kupatiwa huduma za afya na kisaikolojia, kwa msaada wa shirika la Mwezi Mwekundu la Tunisia.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Libya itachukua kundi lililobaki la wahamiaji kati ya 150 na 200. Wizara ya mambo ya ndani ya Libya mapema Alhamisi ilitangaza kufikiwa kwa mkataba wa pande hizo mbili wa kumaliza mzozo wa wahamiaji wasio wa kawaida waliokwama kwenye eneo la mpakani.

Katika taarifa yake baadaye, ilisema kulikuwa hakuna wahamiaji zaidi waliokwama kwenye mpaka kufuatia makubaliano hayo, ikiongezea kwamba doria za pamoja zimeandaliwa ili kulilinda eneo la mpakani.
Mivutano ya rangi imeongezeka nchini Tunisia katika mji wa Sfax baada ya mauaji ya Julai 3 ya mwanamme mmoja raia wa Tunisia kufuatia ugomvi na wahamiaji. Takribani Waafrika weusi 1,200 waliondolewa kwa nguvu na majeshi ya usalama ya Tunisia, na kupelekea kwenye mikoa ya jangwani kwenye mpaka na Libya na Algeria, Human Rights inasema.

Shirika la Mwezi Mwekundu Tunisia Julai 12 liliwapatia makazi kiasi cha wahamiaji 630 waliogundulika huko Ras Jedir, pamoja na wengine 200 ambao walisukumwa kuelekea Algeria.

Kwa mujibu wa kituo cha VOA Swahili, waandishi wa habari wa AFP na vyombo vingine vya habari waliripoti kwamba kiasi cha wahamiaji 350 bado wamekwama huko Ras Jedir katika wiki zilizofuata.

Takribani kilometa 40 kusini mwa Al Assah, mamia ya wahamiaji wengine walionekana kumiminika kuingia nchini Libya, huku wakiwa hawana fursa ya chakula, maji na wala mahitaji muhimu mpaka walipookolewa na walinzi wa mpakani wa Libya mapema mwezi Agosti.

Tangu mwezi Julai, takribani wahamiaji 27 wamegundulika kufariki baada ya kuachwa katika eneo la mpakani kati ya Tunisia na Libya na wengine 73 hawajulikani walipo. Pia mpaka siku ya Jumatano wahamiaji waliendelea kuwasili nchini Libya huko Al Assah kwa kiwango cha takribani watu 50 kwa siku kabla ya kuokolewa na walinzi wa Libya.

Nchi hizo mbili za Afrika Kaskazini ni njia kuu kwa wahamiaji na waomba hifadhi wanaojaribu kufanya safari hatari kwa kutumia boti chakavu kwa matumaini ya kutafuta maisha bora huko Ulaya.

#KonceptTvUpdates

#AFP

Related

HIJA SELEMANI

HIJA SELEMANI

Related Posts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy
BIASHARA

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

by I am Krantz
Sep 22, 2023
DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA
HABARI

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA
HABARI

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA
AFYA

MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST
HABARI

SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO
HABARI

TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

August 2023
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In