ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

UMOJA WA WATANZANIA WALIOTOKA NCHI MBALIMBALI (JATA) WAWEKA MPANGO WA KUWAJENGEA UWEZO WALIOSOMA GEREZANI

Dar es salaam

HIJA SELEMANI by HIJA SELEMANI
Aug 15, 2023
in HABARI
0
UMOJA WA WATANZANIA WALIOTOKA NCHI MBALIMBALI (JATA) WAWEKA MPANGO WA KUWAJENGEA UWEZO WALIOSOMA GEREZANI
0
SHARES
37
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Umoja wa Watanzania waliosoma nchi mbalimbali (JATA) umeweka mpango mkakati wa kipekee wa kuwafikia wale ambao wametoka katika gereza la Kikururu (Gerazani) kwa kuanzisha miradi ya maendeleo inayolenga kuwajengea uwezo wa kuishi kwa kujipatia kipato.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa JATA, Bw. Gregory Mlay, wakati wa kikao kazi cha wanachama kilichofanyika mjini Morogoro, kwa ushirikiano na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA). Kikao hicho kiliwakutanisha viongozi wa Taifa (EXCOM) na viongozi wa kanda za JATA, na kilijadili masuala mbalimbali ya utekelezaji kwa mwaka 2023/2024 na kuimarisha umoja huo.

RelatedPosts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

Oct 2, 2023

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

Oct 2, 2023

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

Oct 2, 2023
Load More

Bw. Mlay alieleza kuwa viongozi kutoka Kanda ya Morogoro, Pwani, Kaskazini, Kusini, Iringa, Kanda ya Ziwa, Kati, na Kanda ya Zanzibar walishiriki kikao hicho. Alisema kuwa katika mwaka huu, umoja huo umeamua kutekeleza miradi sita iliyopitishwa katika mkutano mkuu wa mwaka uliopita (2022), ikiwemo mpango mkakati wa kuwafikia waliotoka gerazani kwa kuwajengea uwezo wa kuishi kwa kuanzisha miradi ya maendeleo.

Mlay alibainisha kuwa hatua nyingine za utekelezaji ni pamoja na kufuatilia na kuwafikia wanachama wa umoja huo waliopo katika kila kanda. “Mpango mkakati wa kuwajengea uwezo waliotoka gerazani ni sehemu ya jitihada zetu za kuboresha hali ya maisha ya watu na kuongeza ufanisi katika jamii,” alieleza Mlay.

Katibu Msaidizi wa Umoja huo, Bibi Edina Ngelageza, aliongeza kuwa pamoja na miradi hiyo sita, kuna miradi mingine inayotekelezwa na wanachama binafsi ambao wamehitimu katika taaluma mbalimbali kama afya, maji, viwanda, mazingira, elimu, na utawala bora. Ngelageza alibainisha mafanikio ya miradi hiyo, ikiwemo mradi wa usafi wa mazingira unaotekelezwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambao umesaidia kuboresha utunzaji wa mazingira nchini.

Mwakilishi wa JICA, Bi. Evona Mathew, alieleza kufurahishwa kwao na jitihada za umoja huo na jinsi inavyosaidia katika kubaini matunda ya ufadhili wao katika sekta mbalimbali. “Hii imekuwa ni njia sahihi ya kufuatilia na kubaini matunda ya ufadhili wa JICA unaoutoa katika sekta mbalimbali kwani unaleta tija katika jamii,” alisema Bi. Evona.

#KonceptTvUpdates

Related

HIJA SELEMANI

HIJA SELEMANI

Related Posts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10
HABARI

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
HABARI

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM
HABARI

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI
BIASHARA

MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA
HABARI

SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA
HABARI

TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

August 2023
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Jul   Sep »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In