ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

I am Krantz by I am Krantz
Sep 4, 2023
in HABARI
0
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
NSSF YAZIDI KUTOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KWA WAJASIRIAMALI, WAHIMIZWA KUJIUNGA NA KUJIWEKEA AKIBA

WAJASIRIAMALI NA WANANCHI WAHAMASIKA, WAJIUNGA NA NSSF

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), umetoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wajasiriamali na wananchi katika Maonesho ya Awali Nguvu Kazi/Jua Afrika Mashariki, katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam ambapo wajasiriamali kutoka Rwanda na Burundi walishiriki.

RelatedPosts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

Oct 2, 2023

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

Oct 2, 2023

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

Oct 2, 2023
Load More

Afisa Mkuu Uhusiano wa NSSF, Janet Ezekiel, amesema NSSF imeshiriki maonesho hayo kwa kishindo kwa lengo la kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wajasiriamali na wananchi.

Amesema baada ya mabadiliko ya sheria ya mwaka 2018, NSSF ilipewa dhamana ya kuangalia sekta binafsi na sekta isiyo rasmi wakiwemo wajasiriamali na wale wote waliojiajiri wenyewe.

“Kulingana na mpango wa Serikali ikaona kwamba hifadhi ya jamii sio kwa wale tu ambao wameajiriwa katika sekta rasmi bali hata wale waliojiajiri katika sekta isiyo rasmi kwa sababu kuna wakati hata wao nguvu zitaisha hivyo watahitaji kupata hifadhi hivyo wakijiunga na kuchangia NSSF watanufaika kwa kupata pensheni ya uzee,” amesema.

Naye, Abdallah Bashiri ambaye ni Afisa Matekelezo wa Sekta isiyo rasmi, akieleza umuhimu wa hifadhi ya jamii, amesema NSSF imeshiriki maonesho hayo kutoa elimu ya hifadhi ya jamii katika makundi mbalimbali kama vile wajasiriamali,  wakulima, wavuvi, wafugaji na wananchi wengine wote.

Amesema NSSF inatekeleza majukumu makuu manne, ikiwemo kuandikisha wanachama kutoka sekta rasmi na sekta isiyo rasmi, kukusanya michango, kuwekeza na kulipa mafao mbalimbali kwa mujibu wa sheria.

Amesema baada ya wajasiriamali kujiandikisha wanapaswa kujichangia kila mwezi kwa ajili ya kesho yao iliyokuwa njema ambapo baadaye Mfuko utawalipa mafao kwa wale watakaojichangia kwa muda wa miaka 15 watalipwa pensheni kila mwezi hadi kufa kwao.

Amesema Mfuko unatoa mafao ya muda mrefu na muda mfupi ambapo mwanachama mwanamke aliyejichangia kwa muda wa miaka mitatu, atakapojifungua atalipwa mafao ya uzazi, pia kwa mwanachama ambaye atafariki pia atanufaika na mafao ya msaada wa mazishi na pia kuna mafao ya matibabu hivyo aliwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo.

Abdallah amesema mwanachama ambaye atajiunga kupitia mpango wa hiari, atapata kitambulisho na atatengenezewa namba ya kumbukumbu ya malipo ‘Control number’ ambayo ataitumia kulipia michango yake.

“Tumeandaa mifumo rafiki na rahisi ambayo itawawezesha wanachama wetu waweze kujiwekea akiba popote walipo,” amesema.

Afisa Mkuu wa Uhusiano na Elimu kwa Umma, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Janet Ezekiel akitoa neno la utangulizi ambapo alisema lengo la NSSF kushiriki maonesho ya Awali Nguvu Kazi/Jua Kali Afrika Mashariki ni kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wajasiriamali na wananchi kwa ujumla.

 
Afisa Mwandamizi sekta isiyo rasmi, Abdallah Bashari akitoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wajasiriamali na wananchi kuhusu umuhimu wa kujichangia kwa ajili ya kutengeneza kesho yao iliyonjema wakati wa maonesho ya Awali Nguvu Kazi/Jua Kali Afrika Mashariki 

Baadhi ya wananchi wakiwa wanajiunga na Mfuko wa Taifa wa Jamii (NSSF), baada ya kupata elimu ya hifadhi ya jamii.

Matukio katika picha

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10
HABARI

KANISA LAPOROMOKA MEXICO NA KUUWA WATU 10

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
HABARI

TAKRIBAN WAHAMIAJI 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 25 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA LORI NCHINI MEXICO

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM
HABARI

AIRPORT YA ZANZIBAR IPO BUSY KULIKO YA DAR ES SALAAM

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI
BIASHARA

MIFUMO YA KIFEDHA KULINDWA ZAIDI

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA
HABARI

SIKU 7 ZATOLEWA MILANGO KUBADILISHWA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023
TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA
HABARI

TWENDE BUTIAMA YAANZA RASMI KUTOKA DAR MPAKA BUTIAMA

by SUZO SHUKRANI
Oct 2, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

September 2023
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Aug   Oct »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In