ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

BETPAWA, POLISI WAUNGANA KUTOA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA BODABODA JIJINI DAR ES SALAAM

SUZO SHUKRANI by SUZO SHUKRANI
Sep 4, 2023
in HABARI
0
BETPAWA, POLISI WAUNGANA KUTOA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA BODABODA JIJINI DAR ES SALAAM
0
SHARES
24
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

RelatedPosts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

Sep 29, 2023

TSO WAZINDUA GALA DINNER

Sep 29, 2023

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

Sep 29, 2023
Load More

Zaidi ya waendesha bodaboda 250 mkoani Dar es Salaam wamenufaika na mafunzo ya usalama barabarani yalioandaliwa na kutolewa na Kampuni ya betPawa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Kitengo cha usalama barabarani.

Mafunzo hayo yamefanyika ijumaa tarehe mosi septemba 2023 yenye ujumbe ‘BetPawa na elimu ya Usalama Barabarani’ yanalenga kuunga mkono jitihada za Serikali za kupiga vita ajali za barabarani zinazoweza kuepukika na ambazo husababisha majeraha na vifo haswa kwa waendesha bodaboda ambao wamekuwa ni moja kati ya kundi linaloathirika sana.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Meneja masoko wa betPawa Tanzania Bi. Borah Ndanyungu alisema takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa bodaboda ni kundi ambalo limekuwa likichangia sana katika ajali za barabarani huku akitaja uelewa mdogo wa sheria za usalama barabarani kuwa moja ya chanzo kikuu cha ajali hizo.

“Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 16,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na ajali za barabarani huku ajali za bodaboda zikichukua nafasi kubwa. Kutokana na ukweli huu, tumeona kuna haja ya kutoa elimu ya usalama barabarani kwa kundi hili ambalo limekuwa ni muhanga wa ajali za barabarani,” amesema Ndanyungu.

Kwa upande wake SP Deus Sokoni ambaye ni Mkuu wa Dawati la Elimu, Kitengo cha Usalama Barabarani kutoka Jeshi la Polisi, aliipongeza kampuni ya kubashiri michezo ya BetPawa kwa kudhamini mafunzo hayo muhimu

 

“Sisi sote kwa pamoja ikiwa ni Pamoja na jeshi la Polisi, madereva, jamii nzima na wadau wote tuna wajibu wa kufanya barabara zetu ziwe salama. Ninayofuraha kuona BetPawa wamekuwa mstari wa mbele na kuamua kufadhili mafunzo haya ambayo yatasaidia sana kundi hili la bodaboda.,

 

Ameongeza kuwa Ajali za barabarani zinsababisha hasara kubwa kwa taifa, familia na jamii kwa ujumla. Hasara hizi ni Pamoja na kupoteza wapendwa wetu ambao wengine tunawategemea, ulemavu wa kudumu pamoja na gharama kubwa za matibabu kwa wahanga wa ajli. Kwa Pamoja tukiungana tunaweza kupunguza sana kama siyo kumaliza kabisa tatizo hili.

 

Mwakilishi wa waendesha bodaboda jijini Dar es Salaam Boniface Mtale alisema ajali za bodaboda zimekuwa zikiongezeka kwa kasi na kufafanua kuwa uelewa mdogo wa sheria na kanuni za usalama barabarani zimekuwa ndiyo chanzo kikuu cha ajali hizo.

 

“Uelewa mdogo wa sheria na kanuni za usalama barabarabi bado ni changamoto kubwa kwa madereva wengi wa bodaboda. Tunawashukuru sana BetPawa  kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kutambua tatizo hili na kuamua kutupatia elimu hii muhimu sana kwetu,” alisema

 

 

 

 

#KonceptTVUpdates

Related

SUZO SHUKRANI

SUZO SHUKRANI

Related Posts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO
HABARI

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TSO WAZINDUA GALA DINNER
HABARI

TSO WAZINDUA GALA DINNER

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
CHANJO YA MBWA NI MUHIMU
AFYA

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN
HABARI

52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA
HABARI

SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 
HABARI

TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 

by I am Krantz
Sep 29, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

September 2023
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Aug    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In