ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NMB yawa benki ya tatu kwa faida Afrika Mashariki

I am Krantz by I am Krantz
Sep 11, 2023
in HABARI
0
NMB yawa benki ya tatu kwa faida Afrika Mashariki
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Benki ya NMB imeshika nafasi ya tatu kwa ukubwa wa faida katika ukanda wa Afrika Mashariki, hii ni kutokana na mafanikio yake kiutendaji hasa ufanisi katika uendeshaji na utoaji wa huduma bora za kibenki nchini.

Katika nusu ya kwanza ya mwaka huu benki hiyo imeweza kutengeneza faida baada ya kodi ya Shilingi Bilioni 262 ikiwa ni ongezeko la asilimia 27 ukilinganisha na nusu ya kwanza ya mwaka 2022.

RelatedPosts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

Sep 22, 2023

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

Sep 21, 2023

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

Sep 21, 2023
Load More

Kutokana na kutengeneza kiasi hicho cha faida, NMB imeweza kushika nafasi ya tatu kwa ukubwa wa faida kati ya mabenki yote ndani ya ukanda huu wa Afrika Mashariki, ikitanguliwa na Benki ya Equity pamoja na Benki ya KCB zote kutoka nchini Kenya ambazo zimepata faida ya TZS bilioni 430 na TZS bilion 264 mtawalia. NMB imepanda kutoka nafasi ya 10 mwaka 2018 hadi kufikia nafasi ya tatu sasa.

Takwimu na uchambuzi wa hivi karibuni wa masoko ya hisa katika ukanda huu unaonyesha kuwa taasisi hiyo kubwa ya fedha nchini yenye mali zenye thamani ya zaidi ya Tsh Trilioni 11 imekua sana kiushindani na kuimarika sokoni katika miaka ya hivi karibuni, huku bei ya hisa zake sokoni ikiongezeka kwa takribani asilimia 28% tangu kutangazwa kwa matokeo yake ya kifedha ya nusu mwaka 2023 hadi kufikia shilingi 4,440 kwa kila hisa Septemba 8 2023.

Kutokana na kufanya vizuri kifedha, mtaji wa Benki ya NMB katika soko la hisa umekua kutoka Tsh 1.38 trilioni mwaka 2018 hadi kufikia mtaji wa kiasi cha Tsh 2.22 trillion Tarehe 8 Septemba 2023, hivyo kuifanya NMB kuwa kampuni ya pili kwa ukubwa katika soko la Tanzania ikitanguliwa na kampuni ya TBL na pia kampuni ya sita kwa ukubwa ndani ya kanda ya Afrika Mashariki, Shelisheli na Mauritus, ikitokea nafasi ya 14 mwaka 2019. Kampuni ya Safaricom Kenya ndiyo inayo ongoza katika ukanda huu ikiwa na mtaji wa zaidi ya shilingi trilioni nne.

Kwa mujibu wa Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi Ruth Zaipuna, mafanikio haya makubwa yanatokana na mazingira wezeshi ya kibiashara yanayowekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na uimara wa uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Bi. Ruth aliongeza kuwa ufanisi wa taasisi hiyo pia umechangiwa na miaka mingi ya ukuaji endelevu pamoja na utekelezaji makini wa mpango mkakati wa uendeshaji wa benki hiyo.

Mwaka 2022, NMB ilipata faida kabla ya kodi ya shilingi bilioni 617 na kuweka historia ya faida kubwa kuwahi kutengenezwa na taasisi yoyote ya fedha nchini. Jarida la Euromoney limeitangaza benki ya NMB kama benki bora Zaidi Tanzania 2023, hii ikiwa ni mara ya 10 ndani ya miaka 11 kwa benki hiyo kubwa kupata tuzo hiyo inayo heshimika duniani kote.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Dkt. Edwin Mhede, alisema wamejipanga kuendelea kuchangia kikamilifu ukuaji wa uchumi wa nchi na ujenzi wa taifa kwa ujumla.

MWISHO…

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy
BIASHARA

Maurel and Prom: Empowering Tanzania’s Sustainable Energy Economy

by I am Krantz
Sep 22, 2023
DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA
HABARI

DR KONGO YATAKA MONUSCO KUONDOKA HARAKA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA
HABARI

HAIER TANZANIA NA AZAM TV WAUNGANA KUKIWASHA KWA PAMOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA
AFYA

MNH YAFANYA UPASUAJI WA KWANZA TUNDU DOGO MOJA

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST
HABARI

SBL KUUNGANISHA TAMADUNI KUPITIA OKTOBA FEST

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023
TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO
HABARI

TAWA YATAKIWA KUJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI MAPATO

by SUZO SHUKRANI
Sep 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

September 2023
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Aug    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In