ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, September 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

TANZANIA YANG’ARA MAONESHO YA 68 YA VITO THAILAND

SUZO SHUKRANI by SUZO SHUKRANI
Sep 7, 2023
in BIASHARA, HABARI
0
TANZANIA YANG’ARA MAONESHO YA 68 YA VITO THAILAND
0
SHARES
23
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Ushiriki wa Tanzania katika Maonesho ya 68 ya Vito na Usonara katika jiji la Bangkok   nchini Thailand umewavutia Wafanyabiashara mbalimbali wa madini kutokana na wengi kutumia malighafi za madini kutoka nchini.

RelatedPosts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

Sep 29, 2023

TSO WAZINDUA GALA DINNER

Sep 29, 2023

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

Sep 29, 2023
Load More

Akizungumza baada ya kushiriki hafla fupi ya ufunguzi wa maonesho hayo jana septemba 6,2023, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo amesema wafanyabiashara wakubwa wa madini nchini humo wakiwemo viongozi wa Serikali wameonesha nia ya kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali zikiwemo  biashara ya madini, uongezaji thamani madini pamoja na kubadilishana uzoefu katika shughuli hizo.

Aidha, Mbibo amesema  uwepo wa Tanzania  katika maonesho hayo ya madini yenye thamani kubwa unalenga  kujifunza pamoja na kuhamasisha urejeshwaji wa minada ya madini nchini na kuhamasisha uwepo wa masoko ya madini ambapo wafanyabiashara hao wanaweza kununua madini kupitia masoko ya madini yaliyoanzishwa katika kila mkoa nchini.

Serikali kupitia Wizara ya Madini inatarajia kurejesha tena minada ya madini nchini pamoja na Maonesho ya Kimataifa ya Vito na Usonara ya Arusha yatakayofanyika kila mwaka kulingana na kalenda za kimataifa ya maonesho ya madini ya vito na biashara za usonara.

Aidha, hivi karibuni Serikali kupitia Tume ya Madini ilitoa taarifa kuwa, Wizara ipo kwenye mchakato wa kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria na Kanuni ili kuwezesha maonesho na minada ya vito kufanyika nchini ikiwemo marekebisho ya Kanuni za Eneo Tengefu la Mirerani za Mwaka 2021 ambazo zilizuia kuuzwa kwa madini ya Tanzanite nje ya Mirerani.

Kufuatia hayo, Mbibo ametoa wito kwa wauzaji, wachimbaji, waongezaji thamani madini kutumia uhusiano  mzuri  uliopo kati ya  Tanzania na Thailand ambao umekuwepo  kwa muda mrefu kuchangamkia fursa  hiyo ikiwemo kuungana na wadau  wa nchi hiyo katika masuala yanayohusu  mnyororo wa shughuli za madini.

Ameongeza kwamba, tayari Serikali ya Awamu ya Sita imefungua milango  ya biashara katika Sekta ya Madini na kuwataka wadau wa madini nchini kutumia fursa hiyo kuwapokea wawekezaji mbalimbali  ili hatimaye  kujenga uchumi imara na kuinua ustawi wa watanzania  kupitia rasilimali madini.

‘’Biashara lazima iwe na wauzaji na wanunuzi wawe tayari kupokea watu wengine na wajifunze namna ya kufanya biashara kutoka biashara ya kitaifa hadi kimataifa kwa madini ya thamani na mawe,’’ amesema Mbibo.

 

 

#KonceptTVUpdates

Related

SUZO SHUKRANI

SUZO SHUKRANI

Related Posts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO
HABARI

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TSO WAZINDUA GALA DINNER
HABARI

TSO WAZINDUA GALA DINNER

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
CHANJO YA MBWA NI MUHIMU
AFYA

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN
HABARI

52 WAFARIKI KWENYE MAADHIMISHO YA MAULID NCHINI PAKISTAN

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA
HABARI

SEKTA YA MADINI YAJA NA MBT KAMA FURSA KWA VIJANA

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 
HABARI

TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 

by I am Krantz
Sep 29, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

September 2023
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Aug    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In